Saturday 5 September 2015

UMOJA NI USHINDI 2015


WAHI MAPEMA  KUMTILIA KURA DR. ALI MOHAMED SHEIN
TAREHE 25/10/2015 ==(READY 2 GO)==

Ahsanteni wananchi wa  Mahonda  
  kwa kuja  kwa  wingi sana na kuujaza uwanja wa Misuka kwenye mkutano  wa hadhara kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.Dr Ali Mohamed  Shein.
DK. SHEIN AWASUTA CUF NA KUSEMA SEMA:
·         TUNAJENGA ZANZIBAR SIO SINGAPORE WALA MAURITIOUS .
·         CUF ELEZENI MAFANIKIO YA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA
·         AWATAKA WASINUNE AKIWAELEZA MAFANIKIO YA SERIKALI NA CHAMA CHAKE
·         ASEMA KUTEKELEZA ILANI YA CCM NDIO MAKUBALIANO


Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi-CCM Dk. Ali Mohamed Shein amesema chama chake na Serikali atakayoiunda endapo atachaguliwa tena amedhamiria kuongeza kasi ya kuijenga Zanzibar ili iweze kufikia malengo yaliyomo katika mipango mbalimbali ya maendeleo ya nchi.
“Tumelenga kuendelea kuijenga Zanzibar kwa kasi zaidi sio Singapore wala Mauritius kwani kazi hiyo tumeianza kipindi kilichopita na tumeonesha kuwa tuna uwezo huo”Dk. Shein ameuambia mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika leo huko Mahonda katika jimbo la Uchaguzi la Donge, Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja.
Amesema katika kipindi kilichopita Serikali aliyoingoza ambayo ilikuwa chini ya Mfumo wa Umoja wa Kitaifa imefanya kazi nzuri ya kuitekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM lakini bahati mbaya wapinzani wanasita kueleza mafanikio katika mikutano yao ya kampeni.
“Tumetekeleza pamoja Ilani ya CCM na baadhi ya wizara zimeongozwa na mawaziri kutoka upinzani lakini katika mikutano yao ya kuomba kura hawataki kuwaeleza wananchi mafanikio tuliyoyapata badala yake wanasema hatujafanya lolote” Dk. Shein alieleza.
Hivyo aliwataka wapinzani kuwa waungwana kwa kutangaza mafanikio ya uongozi wa kipindi cha miaka mitano iliyopita kwa kuwa na wao walishiriki kuyafakisha na kwamba kutekelezwa kwa Ilani ya CCM ndio makubaliano katika kuendesha serikali katika mfumo wa Umoja wa Kitaifa.
Alifafanua kuwa utaratibu tulikubalika ni kuwa Ilani itakayotekelezwa ni ya chama kinachoshinda na hivyo ndivyo ilivyofanyika.
Aliwaeleza maelfu ya wananchi waliokuwa wakikatisha hotuba yake kwa vifijo na vigelegele kuwa Chama cha Mapinduzi kitashinda uchaguzi ujao kwa kuwa kimeonesho weledi na umakini mkubwa katika kupanga na kutekeleza Ilani na kuongeza kuwa katika kampeni zake ni lazima kutangaza mafanikio ya serikali yeke na kunadi Ilani.
Alieleza kuwa wakati katika kipindi kilichopita Serikali imeweza kutekeleza ahadi alizozitoa wakati wa kampeni mwaka 2010, katika kipindi kijacho aliahidi kuongesa kasi ya kuimarisha huduma za jamii.
“Katika miaka mitano ijayo tutazijenga kwa kiwango cha lami barabara za Matemwe-Muyuni, Kichwele-Pangeni, Kinduni-Kichungwani, Mkwajuni-Kijini na Pale -Kiongole” Dk. Shein alizitaja barabara hizo.
Kwa upande wa umeme aliahidi kuvipatia umeme vijiji vya Chechele na Mwmwembe Maji katika jimbo hilo na kususitiza kuwa katika awamu ijayo serikali itaongeza kasi ya usambazaji huduma hiyo vijijini.
Dk. Shein  ataendelea na mikutano yake ya kampeni kisiwani humu kesho ambako atahutubia mkutano mkubwa wa kampeni huko Chwaka. 


VIONGOZI WA CCM Zanzibar wameeleza kuwa CCM ina kila sababu ya ushindi kutokana na kuungwa mkono na wananchi walio wengi nchini hali ambayo inatokana na utekelezaji wake wa Ilani, Sera na ahadi zake kwa vitendo huku wakiwataka wananchi wa Zanzibar kutokubali kurejeshwa walikotoka. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi na wanaCCM uliofanyika uwanja wa Misuka, Jimbo la Donge, Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja, viongozi wa CCM waliohudhuria mkutano huo kwa nyakati tofauti walisema kuna CCM ndio chama pekee kinachojali maslahi wa wananchi. 

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamo wa Pili wa Rais ambaye pia, ni mgombea wa nafasi ya Uwakilishi Jimbo la Mahonda Balozi Seif Ali Iddi alisema kuwa katika chama cha CUF hakuna viongozi wa kuhubiri siasa na badala yake wapo viongozi wasanii. 
Alisema kuwa usanii huo unatokana na kubadilisha maneno kwa kila siku wanapokutana na wafuasi wao ambapo hutumia lugha za kuwadanganya ili wachaguliwe. 

Balozi Seif alishangazwa na hatua zilizochukuliwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad kwenda Tume ya uchaguzi ambapo kutokana na cheo chake haruhusiki kuziingia kazi za Tume hiyo.

Waziri wa Maji, Ardhi na Nishati ambaye pia, ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Ramadhan Abdalla Shaaban nae aliendelea kulielezea suala la mafuta na kuwasisitiza wananchi kutodanganyika juu ya suala hilo.

Waziri Shaaban alisema kuwa CCM na viongozi wake wanahistoria kubwa ya kulifuatialia suala hilo na kueleza kuwa tayari Dk. Shein ameanza kulifanyia kazi kwa mashirikiano na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Nae Balozi Amina Salum Ali alisema kuwa mwaka huu ushindi wa CCM hauepukiki kutokana na hamasa kubwa waliyoipata vijana wa Unguja na Pemba  hatua ambayo inakihakikisha ushindi chama hicho.

Alisema kuwa CCM kila baada ya miaka mitano huchagua viongozi kwa lengo la kutangaza Sera zinazotekelezeka.

Aidha, alieleza kuwa viongozi wa CCM wamefanya mambo mengi ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar na kuwataka vijana na wananchi kwa jumla kuwachagua viongozi wa CCM pamoja na kufahamu azma ya Mapinduzi hatua ambayo matunda yake yanaonekana.

Nae Mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Taifa ambaye pia ni Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Haji Omar Kheir,  alisema kuwa viongozi wa CCM wanachaguliwa kwa sababu wanatekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo na ndio maana wataendelea kuchaguliwa na mwaka huu wataendelea kushinda.

Alisema kuwa wanaogawa pikaka ya Majimbo ni Tume ya Uchaguzi hivyo si haki kukaa kwenye viriri vya mikutano na kuanza kuwalaumu viongozi wa CCM huku akishangazwa na viongozi wa CUF kupita kueleza maneno yasio na msingi.

Aliwataka wananchi na wanaCCM kuwachagua viongozi watakaowaletea maendeleo huku akisisitiza kuwa Dk. Shein ndie atakaepelekwa Ikulu kutokana na busara yake, hekima na anaejua kazi zake za urais.

Alisema kuwa tayari Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa CCM una mpango madhubuti wa wa kujenga Soko jipya la ghorofa litakalojengwa katika Mkoa huo kupitia mradi wa MIVAP.

Nae aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kitope, Makame Mshimba Mbarouk aliwaeleza wananchi na wanaCCM kuwa CCM ni chuo na kueleza kuwa wale wote waliosema kenda UKAWA na wengine kusema kajiunga na chama cha CUF ni maneno yakiupuzi na yasio na maana.

Mshimba alishangazwa na wale wanaosema kuwa CCM haijafanya kitu na kueleza kuwa CCM imefanya mambo mengi huku akisema kuwa amefuatwa sana na wapinzani ili aihame CCM jambo ambalo alisema hawezi kulifanya wala hawezi kukisaliti chama hicho kutokana na kufanya mambo mengi na ataendelea kubaki kwenye chama chake cha CCM, na kuwaombea kura viongozi wote wa CCM.

Nae mama Fatma Karume akiwasalimia wananchi na wanaCCM waliohudhuria katika Mkutano huo na kuwataka wananchi wa Zanzibar kuwa makini na kujua wanatoka wapi na wanakwenda wapi na vijana wakumbuke walikotoka wazee wao na kutokubali kurejeshwa nyuma.

Aliwaambia Wazanzibar kuwa makini katika kuilinda amani iliyokuwepo na kuichagua CCM ili kuepuka yasije kutokezea yanayowakumba wananchi waliokosa amani katika nchi mbali mbali duniani.

Aliwataka wananchi wa jinsia zote na hali zote kuichagua CCM kwani ndicho chama kinachopigania maendeleo yao na kinachowajali.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai aliwaombea kura viongozi wote wa CCM akiwemo Rais wa Zanzibar Dk. Shein, Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dk. John Magufuli pamoja na Wabunge, Wawakilishi na Madiwani.

Nao viongozi wa Mkoa wa Kaskazini kwa nyakati tofauti walisisitiza haja ya kuendelea kusimamia amani na utulivu na kumpongeza Dk. Ali Mohamed Shein kwa kutekeleza vyama Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

 Waliwataka vijana kutohadaika na maneno ya wapinzani na kuwataka wawachague viongozi wa CCM kwani ndio wanaojali maslahi ya wananchi.

Viongozi hao walimueleza Dk. Shein kuwa asiwe na wasi wasi kwa Mkoa wa Kaskazini kwani walifuata maneno ya Mwalimu Nyerere kuwa amani ya Tanzania inatengemea sana kwa kuwepo kwa CCM.


Ahsanteni wananchi wa  Pujini  
 Pemba kwa kuja  kwa  wingi sana na kuujaza uwanja wa Pujini kwenye mkutano  wa hadhara kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.Dr Ali Mohamed  Shein.
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk. Ali Mohamed Shein ameahidi katika kipindi kijacho cha uongozi wake kiwanja cha ndege cha Karume Pemba kitaimarishwa ili kuwezesha ndege za kimataifa kutua moja kwa moja kutoka nje hivyo kuongeza biashara ya utalii nchin.
Ametaja hatua zinazochukuliwa kuwa ni pamoja na ujenzi wa njia ya  ndege na kuongeza urefu na kuweka taa za katika njia ya kurukia na kutua ndege, kuimarisha miundombinu ya huduma za abiria na mizigo kwa kujenga jengo jipya, huduma za umeme na kukamilisha ujenzi wa uzio.
Mgombea huyo wa CCM ametoa ahadi hiyo wakati akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Pujini katika jimbo la uchaguzi la Chonga, wilaya ya Chake Chake, mkoa wa Kusini Pemba. 
Dk. Shein aliwaeleza mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa katika kuimarisha uvuvi nchini Serikali itajenga kiwanda cha kutotolea vifaranga vya samaki huko Beit el Ras Unguja ili kuimarisha ufugaji wa samaki ambao umeanza kushika kasi visiwani humo. 
“Tutajenga chuo cha mafunzo ya uvuvi, viwanda vya kusindika samaki na bandari maalum kwa ajili ya uvuvi Unguja na Pemba” Dk. Shein alifafanua. 
Katika mkutano huo Dk. Shein aliwahakikishia wananchi kuwa uchaguzi utakuwa huru na salama na kwamba wasiwe na hofu yeyote ulinzi na usalama utaimarishwa na kuwaonya wale ambao wamedhamiria kufanya fujo wakati wa uchaguzi. 
“ Tunawahakikishia wananchi kuwa uchaguzi utakuwa huru na wa haki kwani uchaguzi ni utaratibu wa kidemokrasia ambao kila mshiriki anapaswa kuuheshimu” Dk. Shein alisisitiza na kuwatahadharisha wale wote wenye dhamira ya kufanya fujo na kuharibu uchaguzi 
Aliwapongeza wananchi wa Pujini kwa kuwa mstari wa mbele katika ufugaji wa samaki na kubainisha kuwa serikali iligharimia kuanzisha bwawa darasa ili kuwapatia mafunzo ya ufugaji huo. 
Dk. Shein aliwaeleza wafugaji wa samaki wa Pujini kuwa ahadi yake ya kuwapelekea umeme alioitoa wakati alipowatembelea Julai mwaka jana imeanza kutekelezwa ambapo hatua ya awali imeanza kwa kupeleka nguzo. 
Alisema serikali atakayoiongoza katika awamu ijayo itaendelea na mikakati yake ya kuimarisha elimu katika ngazi zote na kuahidi kujenga skuli za msingi kumi za kisasa na za ghorofa kati ya hizo sita zitajengwa Unguja na nne zitajengwa Pemba. 
Katika kipindi kijacho serikali yake itajenga barabara kuu ya kutoka Chake Chake hadi Mkoani na barabara ya Ole hadi Kengeja yenye urefu wa kilomita 35 ambayo maandalizi ya ujenzi yameanza. 
Alizitaja barabara ndogondogo zitakazojengwa kuwa ni Matangini-Kilindi na Kipapo –Mgelema. Kwa upande wa utekelezaji alisema barabara za Chanjamjawiri- Pujini na Kuyuni –Ngomeni kwa kiwango cha kifusi zilikamishwa sambamba na barabara ya Chanjaani-Pujini yenye urefu wa kilomita 5 ambayo ilijengwa kwa kiwango cha lami. 
Kwa upande wa umeme katika kipindi kijacho akichaguliwa tena aliahidi kuvipatia umeme vijiji vya  Limani, Ngomeni, Kitundwini, Chanoni, Mwachawa, Hauraha, Limanda Pujini na Tuunguuni Kilindi. 
Katika kipindi kilichopita aliwaeleza wananchi hao kuwa vijiji vya Kilindi, Banaani, Mtimbu, Kijini na Kibaridi katika jimbo hilo vilipatiwa huduma hiyo. Mgombea huyo wa CCM ataondoka Pemba kesho kurejea Unguja ambako ataendelea na kampeni zake kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa kampeni huko katika viwanja vya Misuka katika jimbo la Uchaguzi la Donge wilaya Kaskazini ‘B’.
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM Dr AliMohamed Shein akiwatambulisha wagombea uongozi wa ngazi mbali mbalin za uongozi katika uchaguzi ujao.

 
 
 
Ahsanteni wananchi wa  Mtambwe Kaskazini 
 Pemba kwa kuja  kwa  wingi sana na kuujaza uwanja wa Mkoongeni kwenye mkutano  wa hadhara kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.Dr Ali Mohamed  Shein.
DK. SHEIN: USHINDI WA CCM MWAKA HUU NI KIFO CHA CUF
  • Wananchi wameamua kuipa kisogo CUF
  • Bei ya soko la dunia ikipanda hatutasita kuongeza bei ya karafuu
  • Nitaendelea kuimarisha mindombinu na huduma za jamii  
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk. Ali Mohamed Shein amesema chama chake kitashinda tena uchaguzi wa mwaka huu na kushika dola na kwamba huo utakuwa mwisho wa Chama cha Wananchi-CUF kwa kuwa chama hicho kimezoea kudanganya wananchi ambao sasa wameamua kukipa kisogo. Katika mkutano wa mkubwa wa kampeni wa chama hicho uliofanyika huko Makoongeni Mtambwe, Dk. Shein aliwaambia wananchi hao kuwa kauli za chama hicho na Katibu Mkuu wake cha kuleta Zanzibar yenye mamlaka kamili ni upotoshaji na ghiliba za kuwafanya wakipigie kura chama hicho lakini kadri muda unavyokwenda wananchi wamekuwa wakizigundua ghiliba hizo. 
“tafsiri ya mamlaka kamili ni kuwa sote tunaukataa Muungano jambo ambalo si kweli na lisilowezekana kwa watanzania wote, Bunge na Baraza la Wawakilishi kuukataa Muungano”alieleza Dk. Shein. 
Mgombea huyo wa CCM aliwataka wananchi wa Mtambwe kufanya uamuzi sasa wa kuwapigia kura wagombea wa CCM na kuahidi kuongeza kasi ya maendeleo katika kipindi kijacho pindi akichaguliwa tena.  
“Tutapiga hatua zaidi ya maendeleo katika kipindi kijacho kwa kuwa katika kipindi kilichopita tumedhihirisha kuwa uwezo wa kufanya hivyo tunao na zaidi washirika wetu wa maendeleo wazidi kuonesha imani kubwa na uongozi wangu hivyo wameahidi kuendelea kushirikiana nasi katika harakati zetu za kujiletea maendeleo” Dk. Shein alieleza.  
Mgombea huyo wa CCM aliwaahidi wapiga kura na wananchi wote kuwa endapo watamchagua tena ndani ya miaka miwili ya mwanzo ya uongozi wake ataondosha michango yote katika sekta ya afya huku akisisitiza kuwa katika kipindi cha mwaka wa kwanza wa uongozi wake kipindi kijacho elimu ya sekondari itakuwa bure.
“dhamira ya serikali ni kuhakikisha malengo ya Mapinduzi ya kutoa afya na elimu bure linatimizwa kadri uwezo wa serikali unavyoimarika.Katika kipindi kijacho tutaendelea kuimarisha huduma za jamii na kwa kuendeleza miundombinu yake na kuzipatia vifaa vya kisasa na wataalamu” Dk. Shein alisema.  
Aliwataka wananchi kuendelea kuimarisha kilimo cha karafuu na kuwataka wasibweteke na kauli za baadhi ya viongozi wa upinzani kuwa mafuta yatachimbwa ndani ya siku 100.
“Mafuta si jambo la leo wala kesho itatuchukua muda mrefu kuchimba mafuta na kufaidika nayo lakini hata kama yatakuwepo bado Zanzibar rasilimali yake kuwa ni zao la karafuu na hatuna budi kulithamini na kulienzi” Dk. Shein alisisitiza. 
Aliwahakikishia tena wakulima wa zao la karafuu kuwa serikali itaendelea kulipa uzito zao hilo na kusisitiza kuwa serikali haitasita kuongeza bei sio tu kuhakikisha wakulima wanafaidika zaidi na zao lakini pia kuhakikisha kuwa zao hilo linaendelea kuwa zao muhimu la uchumi na nembo ya Zanzibar. 
Katika kipindi cha miaka mitano ijayo akichaguliwa Dk. Shein aliahidi kuimarisha miundombinu ya barabara katika jimbo la uchaguzi la Mtamwe na wilaya ya Wete kwa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara za Miembe Mazizi-Chanjaani, Uondwe-Nyali, Mkanjuni-Kivumoni, Mokoongeni-Kinazini na Mkarafuu Mmoja- Mnazi Mmoja. 
“Tulitoa ahadi mwaka 2010 ya kuijenga barabara ya Bahanasa –Mtambwe na nyingine nne zote tumetekeleza.Vituo vya afya vimeimarishwa na kati yao vituo vitatu kati ya hivyo vimepandishwa daraja kuwa daraja la pili hivyo kuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kutoa huduma zaidi kwa wananchi” Dk. Shein aliongeza. 
Kuhusu usambazaji umeme katika jimbo hilo alieleza kuwa ni vijiji vichache tu ndio bado havijapata umeme lakini viwili miongoni mwao vya Chekea kitapata umeme hivi karibuni na mipango itafanywa kukipatia kijiji cha Mtambwe Mkuu huduma hiyo mara tu baada ya kuingia madarakani. 
Mgombea huyo urais kwa tiketi ya CCM ataendelea na kampeni zake kesho kisiwani Pemba kwa kuhutubia mkutano wa kampeni utakaofanyika huko Pujini katika jimbo la uchaguzi la Chonga.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akiwatambulisha wagombe Ubunge katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo kijiji cha Makoongeni Wilaya ya Wete Pemba katika Jimbo la Mtambwe pia kuwaombea Kura Rais wa Jamhuri ya Muungano na Mgombea Mwenza,
WANACCM na wananchi kisiwani Pemba wametakiwa kutotishika na vitisho vinavyotolewa na viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani vya kuwafanyia hujuma siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 25 mwaka huu kwani vyombo vya ulinzi na usalama vimejiapanga kuwalinda katika kutekeleza haki yao hiyo ya kikatiba.

Wakizungumza katika nyakati tofauti katika mkutano wa Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika Mtambwe leo, Mkoa wa Kaskazini Pemba, viongozi wa CCM waliohudhuria mkutano huo walisema vyama vya upinzani vimeshajua kuwa kuna kila dalili kwa CCCM kushinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi huu na kwamba njia pekee inayokusudiwa kufanywa na upinzani ni kutumia vitisho kwa lengo la kuwazuia wapiga kura wa CCM.


Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambaye pia ni Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi amesema Serikali imegundua mbinu zinazokusudiwa kufanywa na vyama vya upinzani na amewahakikishia wanaCCM na wananchi kwamba Serikali imejidhatiti kukabiliana na hali yoyote itakayojitokeza kwa kuweka ulinzi imara ili wananchi wote waweze kuitumia haki yao ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Balozi Seif Ali Iddi aliwataka wananchi wa Mtambwe kuwa makini kusikiliza sera za wagombea kutoka vyama mbali mbali vya siasa lakini kuwachagua wagombea wa CCM ambao ahadi zao zinatekelezeka.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, alishangazwa na kauli za baadhi ya wagombea wenye kunadi maendeleo kwa wapiga kura wakati wao wenyewe wameshindwa kuonesha mfano kwenye vijiji walivyotoka licha ya kuweko madarakani kwa muda mrefu.

Viongozi wa CCM waliopata fursa ya kusalimiana na wananchi pamoja na WanaCCM waliohudhuria katika mkutano huo walielezea kuridhishwa kwao na hali ya mabadiliko na ukuaji wa demokrasia na maendeleo katika jimbo la Mtambwe ambako wananchi wameonesha kuwa huru kuchagua sera za chama wakipendacho wakionesha mabango yanayosomeka "kubadili chama siyo kurtadi".

Alieleza kuwa wimbi kubwa limekuwa linaikimbia CUF na kuipongeza wanaMtambe walio wengi kujiunga na CCM na kuendelea kukiunga mkono kwa nguvu zao zote chama hicho cha CCM.

Akizungumzia maendeleo ya Mtambwe na Pemba kwa jumla, Balozi Seif Ali Iddi alisema kuwa miongoni mwa juhudi zilozofanywa na serikali ndani ya miaka mitano chini ya uongozi wa Dk. Shein ni hatua yake ya kulirejeshea hadhi yake zao la karafuu na kuwapa pencheni wazee waliotimia miaka 70.

Alisema kuwa Dk. Shein ameondosha gharama zilizokuwa zikilipwa na wazazi kaondosha na hivi sasa akina mama watakuwa wakipata huduma hizo bure ambapo pia hivi karibuni aliahidi kuwa akipewa ridhaa atatoa mshahara kima cha chini laki tatu kwani Dk. Shein hadanganyi na anatenda alichoahidi.

Aliwataka wananchi na wanaCCM kuangalia chama kinachotekeleza ahadi zake kwa wananchi huku akisisitiza kuwa ataendelea kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda kwani anauhakika na ushindi hadi pale atakapoamua kupumzika.

Alisema kuwa mbinu zinafanywa ikiwa  ni pamoja na kununua vitambulisho vya CCM,  na kuwaambia kuwa hivi sasa viongozi wa upinzani wanawatisha wananchi kuwa CUF wakishindwa nyumba za wafiasi wa CCM watazichoma moto na kuwataka wananchi kutotishika. na kutokubali kutishwa.

Alisema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama viko macho na kusisitiza kuwa ushindi wa CCM ni lazima mwaka huu, na kuwataka wanaCCM wa Pemba kupamba maskani zao, nyumba zao kwani ushindi kwa CCM hauepukiki.

Aliwataka wananchi kuamka mapema kwenda kupiga kura, na baadae kurudi nyumbani na kuwahakikishia wananchi kuwa kutakuwa na ulizni wa kutosha ili kila mwananchi apige kura kwa amani na utulivu.

Balozi Seif alitoa salamu kwa wananchi wa Kinyikani Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Jimbo la Kojani ambao wameamua kujitoa katika chama cha CUF na kujiunga na CCM kwa kuomba kujengewa barabara yao kutoka Mzambarauni hadi Mchangamdogo.



Nae Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohammed Aboud alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano Djk. Shein amefanya kazia mkubwa ya kuleta maelndeleo, na mfamo ni barabara kutoka Bahanasa kuja Mtambwe.

Alisema kuwa sio tu ujenzi wa barabara, bali ni kuhakikisha wananchi wa Unguja na Pemba wanapata mambo ya msingi ikiwa  ni pamoja na huduma za afya, elimu, maji, umeme, biashara na nyengine kwani amefanya kazi za maendeleo nchini hivyo kuna kila sababu ya kumpa kura za ndio Dk. Ali Mohamed Shein.

Waziri Mohammed alisema kuwa Dk. Shein ni hidaya kwa Zanzibar kwani ni mkweli, mchapa kazi, hana makuu, mwenye subira na mfano wa kuonesha kuwa ameweza kuhimili vituko vingi ambavyo vimefanywa na wapinzani ili kuvuruga amani ambapo Dk. Shein amejitahidi kuhakikisha hilo halitokei.

Alisema kuwa Dk. Shein ameshajenga misingi imarana na amejitahidi katika miaka mitano kwa kuijenga Zanzibar mpya sambamba na kufungua milango ya kuimarisha uwekezaji ili kuhakikisha uchumi unaimarika kwani nia yake ni kuondoa umasikini.

Alisema kuwa uchaguzi sio shwangwe na matusi bali uchaguzi ni takwimu, na tayari kwa upande wa takwimu CCM imejipanga vizru hivyo shangwe hizo ni kazi bure.

Alisema kuwa mara hii CCM haikubali kuibiwa kura zake kisiwani humo kama ilivyozoeleka na kusema kuwa mara hii CCM imejipanga kuhakikisha uporaji wa kura zao unadhibitiwa.

Wapo wafusi wa CUF ambao wameshajua kuwa CUF imeuzwa na wamesema hawakubali kwani chama hicho hakina Mgombea Mwenza.

Aidha, alieleza kuwa chama cha CUF kinajisifu kuwa tayari kimeshawapata ma PO na ma PC ambao watawasaidia katika kufanya vile watakavyowaamuru na kusema kuwa atakaejaribu kuiba kura hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Waziri Aboud alisema kuwa wafusi wa chama hicho cha upinzani wamekuwa wakijisifu kuwa mara hii watahakikisha wanaiba kura na kuitaka Tume ya Uchaguzi kulitambua jambo hilo ambalo ni njia moja wapo ya kuvuruga amani.

Alisema kuwa chama hicho kimejipanga kwa lengo la kuwa wamejipanga kuwa na Mawakala wengi ili kufanya uharibifu mara hii hakuna kugaiwa juisi, maji, pilau kwani mara hii CCM imejipanga vizuri kwa Mawakala wake.
 
Nae Balozi Amina Salum Ali alisema kuwa CCM itaendelea kuuonesha ulimwengu kuwa iko hai na itaendelea kuongoza taifa la Tanzania na kuwataka wanaCCM kuendelea kukiunga mkono chama chao hicho.

Alisema kuwa CUF haina itikadi wala Sera na kushangwazwa kama kweli hayo yapo basi maendeleo makubwa yangeweza kupatikana na kueleza kuwa kinachofanyika ni hadaa.

Alisema kuwa upinzani hawaelewi Utaifa kwani viongozi wa vyma vya upinzani hawawaelezi wananchi na wafuasi wao umuhimu wa Utaifa na badala yake huwatia kasumba kwa lengo la kuichukia Serikali yao.

Alisema kuwa maendeleo yanayotekelezwa na Dk. Shein ni kwa ajili ya wananchi wote na kuwaeleza kuwa hata viongozi wa upinzania wanajua kuwa hakuna maendeleo kama hakuna Sera.

CCM ndio chama pekee kinachoimarisha maendeleo, na kusema kuwa CCM inawajali wananachi wote wa Tanzania na Serikali zote mbili zimekuwa zikileta maendeleo kwa wananchi wote bila ya kuwabagua.

Kwa upande wa akina mama, Balozi amina alisema kuwa akina mama wa Mtambwe wana nguvu ya kuwashawishi akina baba kuiunga mkono CCM ili baadae wasije kujutia na kusisitiza kuwa Dk. Shein amekuwa akihakikisha kuwa maendeleo yanafikiwa na wananchi wote hapa Zanzibar.

Waziri wa Kilimo na Maliasili, Dk. Sira Ubwa Mwamboya alisema kuwa Mtambwe ya leo sio ile ya miaka mitano iliyopita kwani huduma zote muhimu zipo na kushangwazwa na kiongozi wao mkuu Edward KLowasa kudai kuwa akipata uongozi atapeleka elimu, afya na Mamlaka Kamili na kueleza kuwa hayao yote yapo yameshaletwa na CCM.

Aliwataka wananchi kuwapigia kura viongozi wote wanaogombania nafasi kwa upande wa CCM.


Nae Balozi Ali Karume ambaye pia ni Mjumbe wa Halmahsuri Kuu ya CCM aliwataka wanaCCM na  wananchi wa Mtambwe kuwapa kura viongozi wa CCM akiwemo Dk. Ali Mohamed Shein, Dk. Magufuli, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani wa CCM.

Hakuna kitu ambacho unaweza kukitetea kama hukiamini hivyo alisisitiza kuwa ipo haja ya kumchagua Dk. Shein huku akieleza kuwa CCM ina historia kuwa tokea ASP katika suala la ushindi na mwaka huu CCM itaendelea kushinda.

Aliwataka wananchi wa Pemba kutoregeza kamba katika zao la karafuu kwa kudanganyika kuwa kuna mafuta yatakayochimbwa kwa siku mia moja na kueleza kuwa anauhakika na anaamini kuwa Dk. Shein atapandisha tena bei zao la karafuu baada ya kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Zanzibar.

Nao viongozi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba chini ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo Hamad Mberwa walipongeza juhuddi zinazochukuliwa na viongozi wa CCM katika kuimarisha chama hicho huko katika Mkoa wa Kaskaziani Pemba.

Aidha, viongozi hao walitumia futrsa hiyo kuwaeleza historia ya Mtambwe ilivyokuwa hapo kabla na hivi sasa ilivyo kwani maendeleo makubwa yamepatikanwa huko Mtambwe.

Katibu wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba,   alisema kuwa Mtambwe ya sasa ni Mtambwe ya Dijitali na sio ile iliyozoeleka kwani tayari wameshatambua ukweli uko wapi na chama kipi cha kukiunga mkono ili kiwaletee maendeleo.






  Baadhi ya Wananchama wa CCM wakiwa wameshikilia mabango yanayotoa ujumbe "KUBADILI CHAMA SIO KURTADI NA VYAMA HAVIMTII MTU PEPONI YUSEMANE"katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi uliofanyika leo katika kijiji cha Makoongeni Jimbo la Mtambwe Kaskazini Pemba.


Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Shaurimoyo Mkoa
 wa  Mjini Unguja kwa kuja  kwa  wingi sana kwenye mkutano wa hadhara kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM katika uwanja wa Urafiki,jimbo la Shaurimoyo katika wilaya ya mjini Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika leo.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mgombea Urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk. Ali Mohamed Shein ameahidi katika kipindi kijacho akichaguliwa tena atahakikisha kuwa jitihada zaidi zinaelekezwa katika kuimarisha sekta binafsi nchini.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la uchaguzi la Shaurimoyo leo huko katika uwanja wa urafiki Unguja Mjini, Dk. Shein amesema serikali inatambua kuwa haiwezi kufanya kazi pekee hivyo ushirikiano kati ya sekta umma na binafsi ni wa lazima.

“sekta binafsi ni injini ya maendeleo hivyo katika kipindi kijacho mkinichagua tena nitahakikisha sekta hiyo inaimarishwa na ushirikiano kati ya sekta hiyo na sekta ya umma unapewa kipaumbele” Dk. Shein alieleza.

Aidha alibainisha kuwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya sekta hizo ni miongoni mwa mikakati ya Serikali atakayoingoza kuongeza ajira hasa kwa vijana kwa kuwa ushirikiano huo utasaidia katika kuweka na kuimarisha mazingira mazuri zaidi ya kuvutia uwekezaji hivyo kuzalisha nafasi nyingi zaidi za ajira.

Katika mnasaba huo amewataka vijana wasihadaike na ‘porojo’ za baadhi ya wanasiasa wanaowaahidi ajira bila ya kuwa na mpango maalum wa kuzalisha ajira hizo.

“Hawana mpango wowote wanatumia lugha za kuwahadaa ili muwape kura  na lakini Ilani ya CCM inaonesha wazi mipango yake ya kuzalisha ajira na tayari imeonesha kwa vitendo katika kipindi kinachomalizika sasa” Dk. Shein alisisitiza.

Sambamba na ahadi hiyo mgombea huyo wa CCM alisema kupitia Ilani ya chama chake kuwa akichaguliwa tena ataendelea na jitihada za kuimarisha usihirikika kwa kuwapatia mafunzo ya uongozi na uendeshaji wanachama 15,000 wakiwemo viongozi 3,000.

Katika kutatua tatizo la kujaa kwa maji katika baadhi ya maeneo ya jimbo hilo pamoja na maeneo ya jimbo la Kwahani, Dk. Shein aliahidi kuujenga upya mtaro wa maji machafu na mvua katika maeneo hayo ili kuepusha maeneo hayo kujaa maji na hata kusababisha magonjwa ya miripuko.

Kuhusu utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha mwaka 2010-2015, Dk, Shein  alibanisha kuwa ahadi katika jimbo hilo zimetekelezwa ikiwemo uimarishaji wa hospitali ya Mikunguni ambayo pamoja na kutoa matibabu mengine sasa imekuwa kituo kikuu cha matitabu ya macho katika eneo la mjini Unguja.

Katika awamu ijayo ameahidi kutekeleza ombi la wananchi wa jimbo hilo la kupanua hospitali hiyo kwa kuongeza gorofa nyingine lakini hilo aliahidi kulifanyia kazi baada ya wataalamu kuruhusu upanuzi huo.

Katika mkutano huo ambao ulivutia wananchi wengi wa jimbo hilo na maeneo mengine ya mji wa Zanzibar Dk. Shein aliahidi akichaguliwa tena ataendelea na mpango wa kumarisha huduma za jamii ikiwemo maji, afya, elimu na miundombinu ya kiuchumi.

Mjumbe wa Kamati kuuya CCM na Makamo wa Pili wa Rais balozi Seif Ali Iddi akiwasalimia  wananchi na wanaCCM katika Mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi katika uwanja wa mpira Urafiki jimbo la Shaurimoyo Mjini Unguja leo.
Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya Kitaifa ya CCM  Balozi Amina Salim Ali  akitoa salam zake kwa wanachama wa CCM na wananchi wengine waliohudhuria katika Mkutano wa  Kampeni za Uchaguzi zilizofanyika katika kiwanja cha mpira cha Urafiki jimbo la Shauri Moyo kilichopo Wilaya ya Mjini Unguja

Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Nungwi Kaskazini Unguja kwa kuja  kwa  wingi sana kwenye mkutano wa hadhara kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed shein akizungumza na Wanachama wa CCM na Wananchi wapenda amani katika uwaja wa mpira Nungwi Wialaya ya Kaskazini A mkoa wa kaskazini Unguja leo katika mkuatno wa hadhara wa kampeni za uchaguzi mkuu utakaofanyika hivi karibuni.

KAMPENI YA UCHAGUZI NUNGWI
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amehutubia mkutano mkubwa wa aina yake wa kampeni katika mji mdogo wa Nungwi katika mkoa wa Kaskazini Unguja na kuwataka wananchi kukichagua chama hicho kwa kuwa ndicho kinachothamini na kinachotekeleza malengo ya Mapinduzi ya mwaka 1964.
Aliwaambia maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa wanapaswa kuichagua CCM kwani ndicho chama chenye uwezo na kimeonesha mfano wa utekelezaji wa malengo ya Mapinduzi na ahadi za Rais wa kwanza wa Zanzibar hayati Mzee Abeid Amani Karume.
“Mapinduzi ndiyo yaliyoweka msingi wa usawa na kuondosha ubaguzi ambao uliwanyima haki na kuwakandamiza wananchi walio wengi wa Zanzibar” Dk. Shein alieleza.
Katika mnasaba huo alisema kuwa Mapinduzi yalileta usawa na kujenga mazingira ya kuijenga nchi yetu kwa ushirikiano na kwa umoja wetu na kwa maslahi yetu wote.
Mgombea huyo wa CCM alisema Zanzibar ni maarufu ulimwenguni kote tokea karme nyingi zilizopita lakini umaarufu huo hautakuwa na manufaa kwetu endapo hatutaweza kulinda na kuienzi amani na utulivu uliopo.
Katika kipindi kijacho aliahidi kuimarisha huduma za jamii ikiwemo elimu, afya, umeme na maji pamoja na miundombinu ya barabara ili kukidhi mahitaji makubwa ya huduma hizo kutokana na mji huo kupanuka sana kutokana na shughuli za biashara ya utalii.
“Tutaimarisha huduma za umeme kwa kuweka transfoma kubwa yenye KVA 200 katika mji mpya ulioko Ras Nungwi itakayoweza kuhudumia wateja wengi na kwa uhakika zaidi” Dk. Shein alisema na kuongeza kuwa mji huo mdogo utawekewa taa za barabarani hadi Kivunge.
Dk.Shein aliwaeleza wananchi hao kuwa biashara ya utalii ndio inayoipatia Zanzibar fedha nyingi za kigeni hivyo lengo la Serikali katika miaka mitano ijayo ni kuongeza idadi ya watalii wanoitembelea Zanzibar ifikie 500,000 ifikapo 2020 kutoka 300,000 hivi sasa huku jitihada zikielekezwa katika kuimarisha uwezo wa wananchi kitaaluma wa kuweza kuhudumia sekta hiyo. 
Aliwaeleza wananchi hao kuwa kupanua haraka kwa mji Nungwi ni uthibitisho kuwa Nungwi inaendelea kusonga mbele kwa kujenga majengo mengi na hoteli nyingi za kitalii.
Dk. Shein aliahidi atakapochaguliwa tena Serikali yake itawajengea uwezo wavuvi nchini kwa kuwapatia boti zenye ukubwa wa kati na kubwa ili waweze kuvua kwa uhakika na kupata mapato makubwa zaidi.
Kwa upande wa kilimo cha mwani, dk. Shein alisema ataiamarisha masoko la mwani kwa kutafuta masoko mapya ya zao hilo ili wakulima waweze kupata bei nzuri na kufaidi jasho lao.  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
 pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed shein akiteta jambo na Naibu katibu Mkuu wa CCM 
Zanzibar Vuai Ali Vuai wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika  uwanja wa  mpira Nungwi Wilaya 
ya Kaskazini A Mkoa wa Kaskazini Unguja. 
 
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM NEC na Waziri wa ardhi,maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban akielezea wananchi na wanaCCM kuhusu suala zima la Uchimbaji wa mfuta katika mkutano wa hadhara wa 
kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika uwanja wa mpira Nungwi Wilaya ya Kaskazini A Unguja leo.
 Wanachama wa CCM na Wapenda amani wakinyoosha mikono yao juu kuashiria kuunga mkono maneno na sera zilizotolewa na mjumhe wa Kamati Kuu ya CCM Khadija Hassan Aboud leo wakati wa Mkutano wa kampeni za CCM zilizofanyika Nungwi Wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini  Unguja katika uwanja wa mpira.
Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Bumbwini kwa kuja kwa  wingi sana  kwenye mkutano wa hadhara umsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Wananchi na wanachama wa CCM Jimbo la Bumbwini wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa kaskazini Unguja leo,  katika  mkutano   wa hadhara wa kampeni za CCM ulifanyika uwanja wa Skuli ya Bumbwini Makoba ikiwa ni mfulilizo wa mikutano inayoendelea.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk. Ali Mohamed Shein ameahidi kuwa moja ya mambo muhimu atakayasimamia endapo atachaguliwa tena kuiongoza Zanzibar ni kuendelea kuimarisha mazingira ya kuaminiana, kuvumiliana, kupendana na kushirikiana miongoni mwa wananchi wake.

“katika kipindi kilichopita tumefanya kazi kubwa ya kuwaunganisha wananchi kwa kujenga mazingira ya uvumilivu, kuaminiana, kuvumiliana na kushirikiana” Dk. Shein aliuambia mkutano mkubwa wa kamperni huko Bumbwini  Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja.

Alisema kuwa serikali yake atakayoiunda itahakikisha kuwa amani na utulivu Zanzibar inaendelea kuimarika siku hadi siku, miezi hadi na miezi na mwaka hadi mwaka na kusisitiza kuwa hatafanya ajizi katika kuwashughulikia watu wanaotishia amani na utulivu.

“Mimi ni Rais ninayejiamini, wananchi mlinipa kura kuwaongoza na nimekuwa nikitekeleza majukumu yangu ya Urais kwa mujibu wa Katiba na Sheria hivyo hakuna haja ya kutishana katika kuongoza” Dk. Shein alieleza.

Alifafanua kuwa serikali si ya vingozi iwe Rais, Makamu wa Rais, Mawaziri au Makatibu Wakuu bali ni ya wananchi hivyo asitokee kiongozi mmoja kumtisha mwingine kwani kufanya hivyo ni kujidanganya.

“wananchi amueni wenyewe msitishike chagueni viongozi mnaowataka wala msitishike kwani hiyo ni haki yenu ya kikatiba kufanya hivyo” Dk. Shein aliwaambia maelfu ya wananchi hao waliokuwa wakikatisha hotuba yake mara kwa mara.

Katika Mkutano huo uliohutubiwa na makada mbali mbali wa chama hicho,Dk. Shein alieleza hatua kwa hatua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi katika jimbo hilo na kuanisha kuwa katika kipindi kilichopita aliahidi kujenga kituo cha afya Kiongwe ambacho tayari kimejengwa pamoja  na kujenga skuli ya Pangatupu.

Alibasisha kuwa katika kio0jdi kijacho serikali itajenga kitilo cha afya Pangatupu ili kuziweka huduma za afya karibu na wananchi.

Mgombea huyo wa CCM aliahidi kuendelea kuimarisha huduma za jamii katika wilaya hiyo pamoja na miundombinu ya barabara.

Aliwataka wananchi kumchagua tena kushika nafasi ya urais wa Zanzibar na kumchagua Dk John Pombe Magufuli kwa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wagombea wengine wa chama hicho katika nafasi za ubunge na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi.

Dk. Shein ataendelea na kampeni zake kesho kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara huko Nungwi katika mkoa Wilaya ya Kaskazini ‘A’.




 




Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Mkoani kwa kuja kwa
 wingi sana  kwenye mkutano wa hadhara kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM.
   Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na
 Wananchi na wanachama wa CCM Jimbo la Mkoani Mkoa wa kusini Pemba, katika uwanja wa mpira wa Makombeni, mkutano huo wa hadhara wa
 kampeni za CCM ulifanyika leo ikiwa ni mfulilizo wa mikutano inayoendelea.
Mgombea nafasi ya urais kupitia Chama cha Mapinduzi-CCM Dk. Ali Mohamed Shein amesema endapo atachaguliwa tena kuongoza Zanzibar atahakikisha Shirika la Meli na Mamlaka ya Bandari yanaimarishwa kwa kufanyiwa marekebisho makubwa ili kuyawezesha kujiendesha kibiashara kama ilivyofanyika kwa Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC).
Akizngumza katika mkutano wa kampeni huko Makombeni wilaya ya Mkoani, mkoa wa Kusini Pemba leo, Dk. Shein alisema taasisi hizo mbili za serikali ni lazima zijiendeshe kibiashara na kuacha kupokea ruzuku serikalini.
“Baada ya kununua meli kubwa itakayowasili hivi karibuni tutanunua meli nyingine mpya yenye ukubwa kama MV Maendeleo na pia meli nyingine ya mafuta kuchukua nafasi ya MV Ukombozi ambayo pamoja na meli ya MV Maendeleo ya sasa zitauzwa kwa kuwa zimeshapitwa na wakati” alifafanua Dk. Shein.
Kwa upande wa Mamlaka ya Bandari aliwaeleza maelfu ya wananchi waliofika katika mkutano huo kuwa katika kipindi kijacho Serikali itaendelea kuimarisha Mamlaka hiyo kwa kuiwezesha na kuifanya itekeleze majukumu yake kwa ufanisi na kutengeneza faida.
Mgombea huyo wa CCM alisema kuwa ahadi zake kwa majimbo ya wilaya ya Mkoani alizozitoa katika mkutano wa kampeni kama huo tarehe 3 Oktoba 2010 zimetimizwa na kueleza kuwa matengenezo makubwa ya bandari ya Mkoani aliyoahidi yamekamilika.
“Matengenezo ya bandari tumekamilisha na kipindi kijacho tutaiimarisha zaidi kwa kuiwekea vifaa bora” alieleza Dk. Shein na kuonesha kukerwa na kauli za baadhi ya wanasiasa wa upinzani kukejeli bandari hiyo.
“bandari yetu sasa ina uwezo wa kupokea mizigo mingi na lazima tutukuze chetu badala ya kutuza vya wengine,kukejeli jitihada zetu si uungwan” alisema Dk. Shein na kuongeza kwa methali isemayo “usitukane wakunga na uzazi ungaliko”
Alitaja kukamilika kwa ujenzi wa barabara za mkoa wa Kusini Pemba kuonesha utekelezaji wa Ilani ya mwaka 2010-2015 zikiwemo barabara za Mizingani-Wambaa, Mtambile-Kangani, Mtambile-Mwambe,Chajaani– Pujini, Chanjamjawiri-Tundauwa na Mtuhaliwa-Mkanyageni.
Katika mkutano huo uliojaa shamrashamra za wana CCM na wananchi na kuonesha kujiamini kupata ushindi, Dk. Shein aliwaeleza wananchi hao kuwa katika kipindi kijacho jitihada zaidi zitaelekezwa katika kuimarisha ubora wa elimu pamoja na kuendelea kuimarisha miundombinu katika sekta ya elimu.
“Baada ya mafanikio makubwa katika kuimarisha miundombinu katika sekta ya elimu katika kipindi kijacho mazingatio sasa yatawekwa katika kuhakikisha kiwango cha elimu yetu kinaimarika ili watoto wetu wengi zaidi waweze kufaulu kwa madaraja ya juu katika mitihani ya kidato cha nne na cha sita na hatimae kuwawezesha kujiunga na vyuo vikuu kwa wingi” Dk. Shein alifafanua.
Aidha katika kipindi hicho alibainisha kuwa serikali itaimarisha elimu ya watu wazima ili kuongeza kiwango cha wananchi wanaojua kusoma na kuandika kutoka 85 hivi sasa hadi asilimia 95 mwaka 2020.
Kwa upande wa skuli za maandalizi aliendelea kubainisha kuwa katika wilaya ya Mkoani hivi sasa tayari vimejengwa vituo 26 kama alivyoahidi mwaka 2010 na miaka mitano ijayo serikali itajenga vituo vingine 34.
Dk. Shein aliwaeleza kuwa kwa upande wa afya serikali katika kipindi kijacho itavipandisha vituo 38 vya afya kuwa daraja la pili ikiwa ni miongoni mwa hatua za kuimarisha huduma za afya katika wilaya hiyo.
Aliwaeleza wananchi kuwa ujenzi mpya wa hospitali ya Abdalla Mzee unaendelea na hospitali hiyo itakuwa kubwa na ya kisasa. Aitumia fursa ya mkutano huo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping kwa msaada wa ujenzi wa hopsitali hiyo pamoja na kuwezesha ujenzi wa bandari mpya ya Mpigaduri.
Dk.Shein anatarajiwa kuondoka hapa kesho asubuhi kuendelea na kampeni zake kisiwani Uguja ambapo kesho hiyo jionia atahubia mkutanowa kampeni huko Nungwi mkoa wa Kaskazini Unguja. 
 Mjumbe wa Sekretarieti ya kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar Haji Mkema alipokuwa akiwaombea kura Wagombea nafasi za
 Uongozi katika Chama cha Mapinduzi CCM  wakati wa Uchaguzi Mkuu ukifika,katika jimbo la Mkoani katika mkutano wa hadhara wa  kampeni zilizofanyikaleo uwanja wa Makombeni Wilaya ya Mkoani Pemba
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwatambulisha wagombea Udiwani wa CCM kwa Wananchi na wanachama wa CCM Jimbo la Mkoani Mkoa wa kusini Pemba, katika uwanja wa mpira wa Makombeni, wakati wa mkutano  wa hadhara wa kampeni za CCM ulifanyika leo ikiwa ni mfulilizo wa mikutano inayoendelea.

Ahsanteni sana wananchi wa  Jimbo la Kojani kwa kuja  kwa wingi  katika  Kiwanja  cha  Kiuongoni kuja  kumsikiliza Dr Ali Mohamed  Shein  kwenye  kampeni zinazoendelea  Tarehe 3/10/2015.

Mgombea  Urais Rais wa Zanzibar Dr  Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza nawanachama wa CCM,Wananchi wapenda amani waliohudhuria katika  mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM za kuombe kura wagombea nafazi za Uongozi katika Chama hicho,uliofanyika leo uwanja wa Mpira Kijiji cha Kiungoni Jimbo la Kojani Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC pia Waziri wa rdhi,Maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban alipokuwa akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi Jimbo la Kojani Wilaya ya wete Mkoa wa Kaskazini Pemba katika kijiji cha Kiungoni  wakati wa  mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM uliofanyika leo uwanja wa Mpira Kijijini hapo, mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein

Aliyekuwa Balozi Jumuiya ya Nchi za Afrika Nchini Marekeni Bi. Amina Salum Ali alipokuwa akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi Jimbo la Kojani Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba,wakati alipokuwa akiwaombea Kura wagombea nafasi mbali mbali wa CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo uwanja wa Mpira Kijiji cha Kiungoni.
READY 2 GO. Hakuna kurudi nyuma , hakuna kuchelewa.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC Balozi Ali Abeid Amani Karume allipokuwa akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi Jimbo la Kojani Wilaya ya wete Mkoa wa Kaskazini Pemba katika kijiji cha Kiungoni  wakati wa  mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM uliofanyika leo uwanja wa Mpira Kijijini hapo, mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.

Vijana waliojitoa katika Chama cha CUF na kuingia CCM wakinyoosha mikono juu kuonesha ishara ya kuunga mkono chama cha Mapinduzi kwa uwezo wake wakuelezea sera zake kwa Wanachama katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Kiungoni jimbo la Kojani Wilaya ya Wete Pemba leo,yake mbali mbali inayofanyika Unguja na Pemba



Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Gando kwa kuja kwa wingi kumsikiliza mgombea  Urais wa  Zanzibar kupitia 
 Chama Cha  Mapinduzi  Dr Ali Mohamed  Shein leo  hii tarehe 02/10/2015.


 Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CC Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa sera zake wakati wa Mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM zilizoendelea leokatika  uwanja wa mpira kijiji cha Gando Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba

WANANCHI kisiwani Pemba wametakiwa kuwachagua viongozi wa CCM ambao watakaa pamoja na wao na sio wale viongozi wanaowachagua kutoka vyama vya upinzani ambao wakishapata nafasi za uongozi huwakimbia na kutojali matatizo yao.Hayo yalielezwa leo na baadhi ya Viongozi wa CCM Zanzibar, katika Mkutano wa  Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika katika Jimbo la  Gando, Mkoa wa Kaskazini Pemba uliohudhuria na maelfu ya wanaCCM na wananchi ambapo mgeni rasmi alikuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein.Viongozi hao walieleza kuwa viongozi wa vyama vya upinzani wanaochaguliwa na wananchi kisiwani Pemba mara baada ya kupata nafasi za uongozi huhamisha makaazi yao kisiwani humo na kuwasahau waliowachagua.
Katika mkutano huo Balozi Seif alisema kuwa amekuwa akipata amaelezo kutoka kwa wanachama wa CUF kuwa hivi sasa wamechoka kudanganywa na kuwaambia kuwa umefika wakati wa wao kujiunga na CCM."CUF imekuwa sawa na timu ya mpira kila siku ikiingia uwanjani inapigwa mabao hiyo si timu kwa nini wewe ubaki huko njooni CCM Sera zake zinatelezeka tizameni ndani ya miaka mitano ilivyofanya... na karibu tunatengeneza barabara ya Wete- Chake"alisema Balozi.Alisema kuwa Dk. Ali Mohamed Shein amefanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na kutekeleza ahadi ya kununua meli mpaa ambayo itaingia nchi wakati wowote na Dk. Shein ndie atakae izindua.Aidha, alisema kuwa CCM haitaki fujo wala shari huku akishangwaza na mgombea urais wa CUF ambaye ameanza kugombea nafasi hiyo tokea ujana wake.Aliwataka wananchi kujiunga na CCM kwani ni chama ambacho hakijawahi kushindwa.
Nae Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho alitumia fursa hiyo kueleza kuwa miundombinu ya barabara Pemba imeimarika na kutoa shukurani kwa Dk. Shein kwa maendeleo yaliopatikana kisiwa humo. Kificho alisema kuwa Zanzibar imeimarika kutokana na amani iliyopo hatua ambayo imepelekea kukua kwa sekta za maendeleo ikiwemo sekta ya utalii.Aidha, alisema kuwa chama vyama vya upinzani vimekuwa havina hoja kutokana na maendeleo makubwa yaliofikiwa kisiwani humo na ndio maana vimekuwa  havizungumzii kuhusu maji, barabara, umeme, afya, elimu na sekta nyenginezo hiyo ni kutokana na kuwa vyote hivyo vimetekelezwa na Serikali ya CCM.Alieleza kuwa kinachofanywa na vyama hivyo hivi sasa ni kudandia hoja ambazo tayari zimekuwa zikifanyiwa kazi na Serikali kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM chini ya uongozi wa Dk. Shein huku akieleza haja ya Dk. Shein kupewa kura za ndio ili maendeleo zaidi yaweze kupatikana Unguja na Pemba.Aliwataka wananchi hao wa Pemba kutowachagua viongozi ambao mchezo wao ni kukimbia katika vyombo vya kutunga sheria kama walivyofanya katika Baraza la Wawakilishi, Bunge la Katiba na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nae Waziri Kiongozi Mstaafu Shamsi Vuai Nahodha aliwaomba wananchi wa Pemba kujua kuwa viongozi waa CUF wameshindwa kufanya kazi za siasa na kuwaauliza viongozi wa chama hicho hata kujenga madarasa wanasubiri mamlaka kamili.
Aliwataka wananchi wa kisiwa cha Pemba kufanya mabadiliko na kuwachagua viongozi wa CCM kwani viongozi wote waliowachagua katika uchaguzi uliopita




 
 Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Kiwani kwa kuja kwa wingi kumsikiliza mgombea  Urais wa  Zanzibar kupitia 
 Chama Cha  Mapinduzi  Dr Ali Mohamed  Shein leo  hii tarehe 01/10/2015.

DK.SHEIN: KUICHAGUA CCM NI KUJIHAKIKISHIA AMANI, UMOJA, MSHIKAMANO NA MAENDELEO.
Mgombea Urais wa Zanzibar Kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi wa Zanzibar kuwachaguwa wagombea wa chama hicho kwa kuwa mbali ya uwezo wa kuleta maendeleo lakini watawahakikishia amani, utulivu, umoja na mshikamano mambo ambayo ni msingi wa maendeleo ya taifa.
Dk. Shein amewaeleza wananchi wa Kiwani katika jimbo la uchaguzi la Kiwani katika wilaya ya Mkoani kisiwani Pemba kuwa wagombea hao wa urais Dk. John Pombe Magufuli kwa nafasi ya urais wa Serikali la Jamuhuri ya Muungano na yeye kwa nafasi ya urais wa Zanzibar wana uwezo mkubwa wa kutekeleza Ilani ya chama hicho ambayo wamekuwa wakiinadi tangu kuzinduliwa kwa kampeni hizo.
Alizungumzia utelezaji wa Ilani ya kipindi kinachomalizika, mgombea huyo aliwaeleza wananchi hao kuwa katika jimbo hilo ahadi zimetekelezwa kwa asilimia kubwa na kutoa mfano uimarishaji wa huduma za afya.
“Tumetekeleza ahadi zetu kwa vitendo, kituo cha afya Kiwani Tasini tumekijenga na kukamilika, kituo cha zamani Kiwani kimeimarishwa na kituo kipya cha afya kimejengwa katika shehia ya Mtangani” alieleza Dk. Shein.
Katika kipindi cha miaka mitano ijayo alibainisha kuwa huduma za mama na watoto zitaimarishwa na kusisitiza kuwa huduma hizo zitaendelea kuwa bure.
Alisema pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kusambaza umeme vijijini katika wilaya hiyo lakini vijiji zaidi katika shehia ya Kiwani vitapatiwa umeme katika kipindi kijacho ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa usambazaji umeme vijijini.
Katika mkutano huo, Dk. Shein aliahidi katika kuijenga barabara ya Mgagadu Kiwani kwa kiwango cha lami baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha kifusi.
“Barabara hii huko nyuma ilikuwa haipitiki na mtyu alihitajii masaa kutoka Mgagadu hadi huku lakini sasa baada ya kujengwa kwa kuwekewa kifusi hivi sasa inapitika wakati wote bila ya matatizo” Dk. Shein alifafanua.
Mgombea huyo wa CCM aliwataka wananchi kuwachagua pia wagombea ubunge, ujumbe wa Baraza la Wawakilishi pamoja na madiwani wa chama hicho ili kujenga safu kamili ya uongozi wa nchi hivyo kuharakisha maendeleo.


Dk. Shein ataendelea na kampeni zake kesho ambapo atafanya mkutano mkubwa wa kampeni huko Gando Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akionesha Ilani ya Chama kwa wanachama na wananchi wa Chama cha Mapinduzi Jimbo la Kiwani wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba leo alipokuwa akizungumza nao katika mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM zinazoendelea..








Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Paje kwa kuja kwa wingi kumsikiliza mgombea  Urais wa  Zanzibar kupitia 
 Chama Cha  Mapinduzi  Dr Ali Mohamed  Shein leo  hii tarehe 29/9/2015.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

DK.SHEIN SUALA LA MAFUTA LISIPOTOSHWE KWA MANUFAA YA KISASA.


Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema suala la mafuta kutolewa katika mambo ya muungano ni matokeo ya jitihada za pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wake hivyo asitokee mtu au chama kikalitumia suala hilo kama lake binafsi.

“Hakuna haja ya mbwembwe wala kujisifu wote katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano tulishirikiana na kushauriana pamoja kwa muda mrefu hadi kufikia hatua ya kupitisha sheria ya mafuta katika kikao cha Bunge cha mwezi Julai 2015” Dk. Shein alisema.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni huko Paje leo katika jimbo la uchaguzi la Paje, Mkoa wa Kusini Unguja, Dk. Shein amesema wako baadhi ya wanasiasa Zanzibar wanalitumia suala hilo kama mtaji wa kisiasa kwa kuwaeleza wananchi kuwa hatua iliyofikia sasa ni jitihada zao binafsi.

Katika mkutano huo ambao ulivunja rekodi za mahudhurio tangu kufanyika mkutano wa uzinduzi wa kamepeni, Dk. Shein amesema suala hilo limekuwa likipotoshwa kwa makusudi kwa manufaa ya kisiasa hasa wakati huu wa kampeni.

“ningewaelewa wenzangu hawa kama wangewaeleza wananchi kuwa hatua iliyofikiwa ni jitihada za serikali yetu ambao wao ni washirika katika serikali lakini kusema wao ndio waliofanikisha jambo hili inasikitisha na si jambo la kiungwana” Dk. Shein alieleza na kuongeza kuwa kama ni sifa angeweza kujisifu yeye kwani ndie aliyekuwa msimamizi mkuu pamoja na Rais Kikwete.

Alisema yeye amefanya ziara katika nchi za Uholanzi na Ras El Khaima ambako alifanya mazungumzo na kutia saini makubaliano ya awali ya ushirikiano katika kuendeleza sekta hiyo pamoja na kufanya mazungumzo na makampuni mengi yenye azma ya kuja kushiriki katika kuendeleza sekta ya mafuta na gesi.

Dk. Shein alibainisha kuwa baada ya kuwepo makampuni ya kutafuta mafuta Tanzania mwaka 2002 wakati huo akiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alimtuma aliyekuwa Waziri wa Nishati wakati huo Edgar Maokola Majogo kuzungumza na Waziri mwenzake wa Zanzibar wakati huo Burhan Saadat kuhusu suala hilo uchimbaji wa mafuta.

“Majibu ya mashauriano hayo yalikuwa ni kuwa suala hilo lisiharakishwe kwa kuwa linahitaji mashauriano zaidi” Dk. Shein alisimulia na ndipo mazungumzo yalipoanza.

Mgombea huyo wa CCM aliwaeleza wananchi kuwa jitihada za kuliondoa suala la mafuta katika mambo ya muungano lilijadiliwa katika Bunge la Katiba lakini baada ya kuwa mchakato huo haukukamilika yeye na Rais wa Jamhuri ya Muungano walilipeleka suala hilo kwa wanasheria wakuu ili kutumia bunge kulikamilisha na ndivyo lilivyofanyika.

“Ilikuwa ni busara yetu viongozi kulipelekea suala hili kwa wanasheria wetu wakuu baadae tukalijadili katika vikao vyetu hadi sheria kupitishwa bungeni” Dk. Shein alisisitiza.

Hata hivyo aliongeza kuwa ni jambo la kushangaza watu hao wanaojinasibu kuwa wamefanikisha suala hilo ndio hao hao waliopinga suala hilo na kukimbia bungeni wakati sheria ya mafuta ilipokuwa ikipitishwa. 

Akibainisha zaidi Dk. Shein kuwa wakati hayo yakiendelea huku Serikali ya Zanzibar ilikuwa ikitayarisha sera yake na kudokeza kuwa imekamilika pamoja na kwamba rasimu ya sheria iko tayari ikisubiri kupitishwa katika Baraza la Wawakilishi ili kazi ya kuendeleza sekta ya mafuta na gesi ianze kwa kasi.

Aliwataka wananchi wasihadaike na maneno ya viongozi hao kuwa uchimbaji huo utaanza mara moja na kuwatahadharisha kuwa hadi kuyachimba mafuta itachukua sio chini ya miaka mitano.

Mgombea  Urais wa  Zanzibar  kwa  tiketi ya  Chama Cha  mapinduzi  Dr  Ali Mohamed  Shein akiwahutubia  malaki ya wananchi waliofurika katika Uwanja wa Paje  Jimbo la  Paje kwenye mkutano wa  kampeni ya kuomba  ridhaaa ya kuongoza  tena  Zanzibar. Kwa  ridhaaa  yao  wananchi wa  Paje  wamekubali  kumpa  kura  zote  yeye  na  wagombea  wote wa CCM kuanzia  mgombea  Urais  wa  Tanzania , wabunge , wawakilishi  na  wadiwani.
DK. SHEIN: NICHAGUENI TENA TUENDELEE KUSHIRIKIANA KWA KUONGEZA KASI YA KUIJENGA ZANZIBAR.

Mgombea wa nafasi ya urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi kumpa tena fursa ya kuongoza ili waendelee kushirikiana kuijenga Zanzibar.

Amesema katika kipindi cha miaka mitano kinachomalizika sasa Zanzibar imepiga hatua kubwa kimaendeleo kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM hivyo kumchagua tena yeye na chama chake kuongoza ni fursa nyingine kwa wananchi wa Zanzibar kuendeleza kasi ya maendeleo ya nchi yao.

Katika mkutano wa kampeni uliofanyika huko Paje katika jimbo la uchaguzi la Paje,Mkoa wa Kusini Unguja, mgombea huyo wa CCM aliueleza umati mkubwa wa wananchi ambao haujawahi kutokea kuwa ahadi alizozitoa kwa jimbo hilo katika mkutano wa kampeni kama huo mwaka 2010 zimetekelezwa na kuahidi kuongeza kasi ya utekelezaji wa Ilani mpya ya chama hicho ya mwaka 2015-2020.

“Tumetekeleza Ilani yetu kama tulivyopanga katika sekta ya afya, elimu, maji, umeme na sekta ya utalii”na kuongeza kuwa kwa sekta ya barabara utekelezaji umeanza na utakamilishwa katika kipindi kijacho.

Alifafanua kuwa baada ya kukamilisha kuifanya hospitali ya Makunduchi kuwa ya wilaya, Serikali itaendelea kuimarisha huduma za afya katika mkoa huo kwa kuiimarisha hospitali ya Kivunge na kituo cha afya cha Paje kwa kivipatia vifaa na wataalamu wa afya.

“Kazi ya kuipandisha hospitali ya Makunduchi kuwa ya wilaya imekamilika kwa kuiwekea vifaa vipya na kuwapatia madaktari wakiwemo kutoka nje ya nchi na tunatarajia kuongeza majengo mengine mapya kuiwezesha hospitali hiyo kuwahudumia watu wengi zaidi” alieleza Dk. Shein na kuongeza kuwa hivi sasa hata wananchi wa mjini wanafika katika hospitali hiyo kufuata huduma.

Aliongeza kuwa Serikali hivi karibuni ilifungua kituo kipya cha afya huko Kajengwa Makunduchi ikiwa ni sehemu utekelezaji wa mpango wa Serikali wa uimarishaji wa huduma za afya nchini.

Dk. Shein aliwaeleza wananchi hao kuwa katika kipindi kijacho Serikali itajenga dakhalia katika skuli ya sekondari Paje Mtule ambayo ni skuli mpya ya kisasa ambayo imejengwa ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya mwaka 2010 -2015 ya kuimarisha elimu nchini.

Katika kuendelea kuimarisha elimu, Dk. Shein ameahidi katika kipindi cha miaka mitano ijayo kuzipatia skuli zote za sekondari kompyuta ili ziweze kwenda na mabadiliko ya sayansi na tekinolojia.

Kuhusu ahadi ya kusambaza umeme vijijini, Dk. Shein alieleza kuwa  utekelezaji wake umezidi asilimia mia na kwa upande wa Paje ni maeneo machache yaliyobaki na kuahidi kukamilishwa muda mfupi ujao baada Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) kwa kuweka transfoma mpya.Mgombea huyo wa CCM anatarajiwa kwenda Pemba kuendelea na kampeni zake kesho.

Balozi  Seif  Ali Iddi  akiwahutubia  wananchi katika mkutano huo. 
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar na mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Waziri Kiongozi mstaafu wa zanzibar pia mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Shamsi vuai Nahodha wakati alipowasili katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Paje Jimbola paje Wilaya ya Kusini Unguja.

Mzee Kwacha akiwahutubia wananchi waliojaa  sana kupita kiasi  katika Uwanja wa  Paje.
  


 Baadhi ya Viongozi wa   CCM wakiwa katika mkutano wa CCM katika kampeni zinazoendelea wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CC Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akitoa sera katika mkutano wa CCM uliofanyika jimbo la Paje katika kijiji cha Paje Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja leo.
 
 
 
Baadhi ya wananchi na wanachama cha Mapinduzi CCM wakiwangalia kikundi cha sarakasi kikitoa burudani wakati wa mkutano wa CCM uliofanyika leo jimbo la Paje uwanja wa mpira Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja katika kampeni zinazoendelea
 
Ahsanteni wananchi wa Jimbo la Mtopepo katika Uwanja wa  Garagara kwa kuja kwa wingi kumsikiliza mgombea  Urais wa  Zanzibar kupitia 
 Chama Cha  Mapinduzi  Dr Ali Mohamed  Shein leo  hii tarehe 28/9/2015.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Magharibi Unguja CCM Yussuf Mohamed Yussuf wakati wa Mkutano wa hadhara kampeni za CCM jimbo la Mtopepo   katika uwanja wa Garagara Wilaya ya Magharibi A Unguja leo.
VIONGOZI wa CCM Zanzibar wamewataka wananchi wa Zanzibar kuendeleza amani, utulivu na mshikamano uliopo na kuwaonya wale wote wanaokusudia kufanya vurugu wakati wa uchaguzi mkuu wajue kuwa Serikali pamoja na vyombo vyake vya Dola viko macho. Viongozi hao waliyasema hayo leo katika Mkutano wa  Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika katika uwanja wa Garagara, Jimbo la Mtopepo, Mkoa wa Mjini  Magharibi uliohudhuria na maelfu ya wanaCCM na wananchi ambapo mgeni rasmi alikuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein.
 
Nae Mjumbe wa Kamati Kuu na Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd alisema kuwa vyama vya upinzani hawana Sera na hoja na hivi sasa wamebaki kubwabwaja.
Balozi Seif alisisitiza haja ya kuimarishwa kwa umoja na mshikamano kwa wananchi na wanaCCM kwa jumla na kusema kuwa umoja ndio silaha ya kushinda kwa CCM. 
Alisema kuwa kuwepo kwa amani na utulivu ni jambo la lazima na kuwaonya wale wote waliodhamiria kufanya fujo wakati wa uchaguzi kuachana na azma yao hiyo na kuwaonya wanachama wa CUF wasije kujaribu kufanya fujo huku akiwataka wazee wa Darajabovu kutowaachia vijana wao kufanya fujo. 
Aidha, Balozi Seif aliwataka wazee wasije kuilaumu Serikali iwapo watoto wao watafanya fujo kwani Dola haijaribiwi wala haichezewi na kueleza kuwa anaetaka kujaribu akale muhogo ajue kama ni mtamu ama mchungu lakini sio serikali. 
Alisema kuwa Serikali iko macho kwa kuwadhibiti wale wote walio na lengo la kufanya vurugu siku ya tarehe 25 na 26. Alisema kuwa huu si wakati wa kuwasemea wananchi, na hakuna serikali ya mkataba kwani serikali ya mkataba lengo  lake ni kuvunja Muungano, na CCM haiko tayari kuwepo kwa serikali ya Mkataba na kueleza kuwa CCM wanachokijua wao ni serikali mbili.  
Nae Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho alitumia fursa hiyo kwa kusema kuwa Dk. Shein ni mtu muadilifu, makini, muangalifu na katika maamuzi yake hakurupuki na kwa mwenendo na tabia hizo hakuna mgombea wa urais wa kumpa kura nyingi za ndio isipokuwa Dk. Shein.Kificho aliwaomba wananchi kuwapeleka Wawakilishi wa CCM na Wabunge wa CCM kwani wao ndio wanaofanya kazi vizuri kwa maendeleo ya Watanzania na wananchi wa Zanzibar kwa jumla na hawana mtindo wa kutoka toka katika nyumba hizo za kutunga sheria.
 
Nae Waziri wa Maji,Ardhi na Nishati Ramadhani Abdalla Shaaban  alishangazwa na kauli za CUF zinazosema kuwa  ndani ya miaka 50 Zanzibar haina maendeleo na kusema kuwa mbali ya miaka hiyo wanayosema wapinzani tayari ndani ya miaka mitano tu ya Dk. Shein maendeleo yaliopatikana Unguja na Pemba ni makubwa.Alieleza kuwa tayari wanaCCM na wananchi wameshaamua tarehe 25 kummiminia kura zote Dk. Shein na kusema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya CCM uchumi umeimarika. 
Pamoja na hayo, alieleza kuwa  angalau CUF wanakiri kuwa kifungu cha Katiba mpya inayopendekezwa cha 23 na 26 kimeelezea kwamba ardhi, mafuta na gesi yatashughulikiwa na Zanzibar, na kusema kuwa kinachosubiriwa ni wakati wa kuipigia kura Katiba inayopendekezwa ifanye kazi. 
Alisema kuwa tayari Rais Jakaya Mrisho Kikwete na  Dk. Shein wameshakubaliana juu ya Sheria ya mafuta na gesi, na tayari sheria hiyo imeshakwenda kwenye Bunge la Muungano kwa lengo la kuwa Zanzibar ishughulikie wenyewe rasilimali hizo.
Nae Bi Fatma Karume mke wa muasisi wa Zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume, alisema kuwa wanawake walidhalilishwa, walitupwa lakini ASP ikaliona hilo na hatimae kuwasimamisha akina mama kwenda katika mikutano ya hadhara na kupiga kura kwani hapo mwanzo hawakupewa fursa hizo. 
Bi Fatma, alitoa pongezi kwa akina mama kwa kupokea wito na kujitokeza kwa wingi katika mikutano  ya Kampeni ya CCM ambapo alitumia fursa hiyo kumuombea kuwa Dk. Shein, Dk. Magufuli, Samia, Wabunge, Wawakilishi pamoja na Madiwani wote huku akieleza kuwa Zanzibar tayari imeshakuwa huru tokea  Januari 12, 1964. 

Nae Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mfenesini Yussuf Mohammed Yussuf aliwataka wanaCCM kuzitunza shahada zao za kupigia kura na kuwataka kuwapigia kura wagombea wote wa CCM.Alisema kuwa CUF hawana hoja na kushangazwa na kauli inayotoa kuwa Zanzibar haina Mamlaka kamili wakati tayari Zanzibar inayo mamlaka Kamili ila nia ya chama hicho ni kurudisha uongozi wa Kifalme.
  
 

 
 
 Ahsanteni wananchi wa Mkokotoni kwa kuja kwa wingi kumsikiliza mgombea  Urais wa  Zanzibar kupitia  Chama Cha  Mapinduzi 
Dr Ali Mohamed  Shein.
Mgombea  Urais wa Zanzibar kwa  tiketi ya  CCM Dr  Ali Mohamed  Shein akiwahutumia wana CCM waliofika kwenye kiwanja cha  Mkokotoni kwenye mkutano wa  kampeni ya uchaguzi mkuu  tarehe 27/9/2015.


VIONGOZI wa CCM Zanzibar wameeleza kuwa hoja inayotolewa na chama cha CUF ya kutaka kuleta Mamlaka Kamili ni dhamira ya kumrejesha Sultan kuja kuiongoza Zanzibar kwa njia ya mlango wa nyuma.

Viongozi hao waliyasema hayo leo katika Mkutano wa  Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika katika uwanja wa Sun Rise, Mkokotoni, Mkoa wa Kaskazini Unguja uliohudhuria na maelfu ya wanaCCM na wananchi ambapo mgeni rasmi alikuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein.

Alisema kuwa CUF hawana hoja na kushangazwa na kauli inayotoa kuwa Zanzibar haina Mamlaka kamili wakati tayari Zanzibar inayo mamlaka Kamili ila nia ya chama hicho ni kurudisha uongozi wa Kifalme.

Alisema kuwa viongozi wa CUF wameishiwa hoja na hawana la kuwaambia wafuasi wao na hivi sasa wamekuwa wakitumia jina lake kwa kunokesha mikutano yao. "labda kwa kwa sababu mimi mweusi na siwezi kujifanya mweupe kama Jusa",alisema Balozi Seif.

 "Kama mimi mweusi ndio alivyoniumba Mungu sasa na wale waliokuwa na vilema visivyoonekana inakuwaje",alisema Balozi na kueleza mwaka huu CUF wanaanguka  huku akisisitiza kuwa Serikali inatolewa kwa nguvu za kura.

Aidha, Balozi Seif Ali Idd, alisema kuwa CUF hawana ajenda na liliopo hivi sasa ni kubwabwaja na kuwaeleza wanaCCM kilichobaki ni kwenda kupiga kura tarehe 25 mwezi huu, na CCM kupata ushindi na kueleza kuwa CUF haina ubavu wa kuishinda CCM.

Balozi Seif alisema kuwa tayari chama cha CUF wanajua kuwa mara hii wanashindwa na  ndio maana wamekuwa wakipita kununua vitambulisho vya kupigia kura kwa wanaCCM.

Alieleza kuwa mikakati wanayopaka ya kufanya vurugu Oktoba 24, 25 na 26, tayari imeshajulikanwa na kutumia fursa hiyo kuwata wazee wa CUF wa Mkoa wa Kaskazini kutowaachia watoto wao kufanya vurugu na kusema kuwa vyombo vya dola havichezewi na kuwataka wasije wakailaumu Serikali na kutowaachia watoto wao kuingia mtegoni, wasije kufanya vuru, wala maandamano.

Alisema kuwa mambo mengi ya vurugu wanayokusudia kufanya CUF wanayajua na wana ushahidi nayo na huku akieleza kuwa ipo siku watayatoa. "Chokochoko kachokoe pweza...CCM haichokolewi iko imara na ukifanya mchezo itakushughulikia",alisema Balozi Seif.

Alisema kuwa Oktoba 25  mwaka huu ni siku ya ushindi wa CCM hivyo kila mmoja aende mapema kupiga kura na kuwahakikishia wananchi kuwa siku ya uchaguzi ulinzi wa kutosha utakuwepo kwa ajili yao na watalindwa wakati wote.

Nae Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Kiongozi Mstaafu Shamsi Vuai Nahodha alisema kuwa Mamlaka kamili ya Zanzinar yalipatikanwa tokea mwaka 1964 chini ya Marehemu Mzee Abeid Karume na hakuna mtu yeyote wala kikundi chochote cha watu ambacho kina uwezo wa kufanya hivyo hivi leo.

Alisema kuwa wanachokusudia kukifanya chama hicho kwa kutaka Zanzibar iwe mwanachama wa Umoja wa Mataifa, iwe na safaru yake, Wizara yake ya mambo ya nje yake ni jambo la kushangazwa kwani taifa lolote duniani haliwezi kuwa na viti viwili katika umoja wa Mataifa wala haiwezekani kuwa na sarafu mbili wala Wizara mbili za Mambo ya nje ndani ya taifa moja.

Shamsi aliendelea kuwashangazwa na CUF kutaka kuanzisha Mamlaka kamili na kueleza kuwa  chama hicho na kile cha CHADEMA msiimamo wao unafanana lakini dhamira zinatofautiana kwani lengo lao ni kuvunja Muungano kwa kutumia lugha ya ulaghai.



Alisema kuwa dhamira ya CHADEMA ni kuwarubuni CUF ili kuwaunga mkono na kuwa na mgombea mmoja wa Jamhuri ya Muungano na la kusikitisha zaidi ni kuwa CHADEMA kimefanikiwa, kuvidhoofisha vyama vya CUF na NSSR MAGEUZI. Pia alieleza kuwa CCM itaendelea kuunga mkono sera ya Serikali mbili.

Alieleza kuwa CCM inaamini kuwa Sera ya Serikali mbili ndio yenye uwezo wa kuongoza serikali, na kusisitiza kuwa Sera ya Serikali tatu haina uwezo wa kuulinda Muungano wala kuyalinda Mapinduzi ya Januari 12, 1964.

Kwa upande wa Muungano alisema kuwa Wazanzibari wamekuwa wakinufaika na Muungano na kueleza kuwa Tanzania Bara wapo Wazanzibari wanaopata huduma kadhaa za maisha ya mwanaadamu ikiwemo ardhi, maji safi na salama na huduma  nyenginezo bila ya bughudha.

Shamsi alishangazwa na wale wote wanaosema kuwa Muungano hauna maana na kueleza kuwa ipo haja ya kutafuta mada nyengine na sio hiyo.

Akieleza juu ya vitendo vinavyofanywa na viongozi wa CUF, alisema kuwa wapo wanachama na viongozi wanapita kwenye Majimbo kununua vitambulisho vya kupigia kura na kueleza kuwa Sheria ya uchaguzi inasema kuwa mwananchi yeyote wa Zanzibar aliesajiliwa kwenye Daftari, haijalishi kuwa shahada yake, imepotea ama imenunuliwa au imeibiwa, ana haki ya kupiga kura.

Hivyo aliiomba Tume ya Uchaguzi kuhakikisha kila Mzanzibari mwenye Shahada na asie na shahada wakati jina lake limo kwenye Daftari la kupiga kura ipewe fursa hiyo.

Nae Bi Amina Salum Ali aliwataka wananchi wa Kaskaznini kutobabaishwa na maneno ya wapinzani huku akieleza miongoni mwa mafanikio yaliopatikana katika Mkoa huo ikiwa ni pamoja na uimarishwaji wa miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyengine za kijamii.

Aidha, aliendelea kueleza kufarajika kwake na mipango ya Dk. Shein ya kuimarisha sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha Zanzibar inalima na kuzalisha mchele wake wenyewe.

Nae Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Haji Omar Kheir ambaye pia ni mgombea Uwakilisgi Jimbo la Tumbatu,alisema kuwa WanaCCM wanasubiri siku ya tarehe 25 Oktoba mwaka huu kukirejesha madarakani chama hicho.

Mapema Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Haji Juma Haji, alisikitishwa na kauli za chama cha CUF zinazoelezwa katika mikutano yao kuwa Zanzibar itaongozwa na wale walioondoshwa mwaka 1964 pamoja na kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali hiyo itaingia madarakani na wale wote waliochukuliwa mashamba yao wanawarudishiwa mashamba yao kwani yamechukuliwa kwa dhulma.

Alieleza kuwa wanaCCM wanaamini kuwa uchaguzi wa mwaka huu utakuwa wa huru, haki na amani, na kusema kuwa vitendo vinavyofanywa na CUF katika Mkoa huo hawaridhiki kwani wameanza kuchana picha za wagombea wa CCM na kuwataka vijana wa Mkoa wa Kaskazini wasikubali kutumiwa na CUF kufanya hivyo.

Alisisitiza kuwa Mkoa wa Kaskazini ushindi hauna mbadala, huku akishangazwa wale wanaoparamia miti na kuanza kuchana picha za wagombea wa  CCM"Waanaparamia miti kwaru kwaru utazani kima wanagombana na picha zisizosema waje kugombana na mimi Haji Juma nnosema',alisema  Haji.
  
 
 


Ahsanteni   wananchi kwa kuwa pamoja kwenye sala ya  Eid na  Baraza la  eid hapo Mkokotoni. Mungu atujaalie Zanzibar yenye kuendelea na amani na baraka tele. Kesho tarehe 27 tunakuja tena Mkokotoni  tuwe pamoja kumsikiliza mgombea urais urais wa  Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein katika kampeni za uchaguzi mkuu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dr Ali Mohamed  Shein akiwahutumia wananchi katika Baraza la  Eid katika sikukuu hii ya mfungo tatu iliofanyika Mkokotoni Kaskazini Zanzibar.
HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHE. AL-HAJJ DK. ALI MOHAMED SHEIN, KATIKA
BARAZA LA IDD- EL-HAJJ: 24 SEPTEMBA, 2015
SAWA NA MWEZI 10 MFUNGUO TATU, 1436 HIJRIA

BISMILLAH RAHMAN RAHIM

Naanza kwa kushuhudia kuwa hapana Mola anayestahiki kuabudiwa kwa haki na viumbe vyote isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhana Wataala.  Yeye ndiye Muumba wa Dunia na Akhera na kwake Yeye ndiyo marejeo ya viumbe vyote.  Tunakiri kwa kauli na kuitakidi kwa moyo kuwa Mtume Muhammad (S.A.W) ni Mtume wake wa haki na kigezo chema cha uchamungu kwa waumini sote.
Rehema na amani ya Mwenyezi Mungu zimshukie Mtukufu wa daraja na mbora wa viumbe; Sayyidna Muhammad (S.A.W), Aali na Sahaba zake pamoja na waumini wote waliofuata njia yake ya uongofu hadi siku ya kiama.  Tumuombe Mola wetu (SW) atujaalie na sisi tulio hai, ndugu, jamaa na wale wote waliokwishatangulia mbele ya haki tuwe miongoni mwao.  Atupe ubainifu wa kuyafanya mambo ya kheri  na tuyaepuke mambo ya shari na maovu, ili tuweze kufanikiwa hapa Duniani na huko Akhera tuendako.  Amin!
Mheshimiwa Sheikh Khamis Haji Khamis;
Kadhi Mkuu wa Zanzibar.
Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad;
Makamu wa Kwanza wa Rais,
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi;
Makamu wa Pili wa Rais,
Mheshimiwa Dk. Amani Abeid Karume,
Rais Mstaafu wa Zanzibar;
Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho;
Spika wa Baraza la Wawakilishi,
Mheshimiwa Omar Othman Makungu;
Jaji Mkuu wa Zanzibar,
Waheshimiwa Mawaziri,
Waheshimiwa Mabalozi,
Wageni Waalikwa,
Ndugu Wananchi,
Mabibi na Mabwana,

Assalamu Aleikum Warahmatullahi Wabarakatuh

IDDI MUBARAK
Ndugu Wananchi,
Nimeanza hotuba yangu kwa kumtukuza Mola wetu (SW) na kukiri kuwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) ni Mtume wa haki wa Mwenyezi Mungu ambaye ni wajibu wetu kumsalia, kuyazingatia na kuyafuata mafundisho yake ili tuweze kufanikiwa katika kuyatekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu na tujiepushe na yale yote tunayokatazwa kuyafanya. Kupitia mafundisho ya Mtume (S.A.W) kutoka kwa Mwenyezi Mungu, tumetakiwa tuitekeleze ibada ya Hijja kwa kila mwenye uwezo katika nyumba tukufu iliyopo Makka huko Saud Arabia.  Mwenyezi Mungu katika aya ya 97 ya Surat Aali Imran anatufahamisha uzito na umuhimu wa kuitekeleza ibada ya Hijja kwa kusema:
“Na kwa ajili ya Mwenyezi Mungu imewawajibikia watu wafanye Hijja katika nyumba hiyo, kwa yule awezaye kwenda huko.  Na atakayekufuru (atakayekanusha) basi Mwenyezi Mungu si muhitaji kuwahitaji walimwengu”.
Ndugu Wananchi,
Leo tunaungana katika furaha ya sikukuu ya Idd el Hajj na waislamu wenzetu kwa maelfu kutoka mataifa mbali mbali, wa rangi na hadhi mbali mbali walioitikia wito wa Mola wetu kwenda kuitekeleza Ibada ya Hijja katika mji Mtukufu wa Makka.  Kwa hakika, hii ni neema kubwa kwetu kwani wapo wenzetu wengi miongoni mwetu ambao hawakuweza kuifikia siku hii.  Kwa hivyo, ni wajibu wetu kumshukuru Mola wetu kwa kuturuzuku neema hii ya kuifikia siku hii,  ambapo ni miezi michache tu iliyopita, tulijaaliwa kuisherehekea sikukuu ya Idd-el-Fitri kwa amani na salama.  Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaaliya siku hizi za furaha na kuwa pamoja katika kuzisherehekea.
Ndugu Wananchi,
Ni jambo la kutia moyo na kumshukuru Mwenyezi Mungu kuona kwamba idadi ya mahujaji wa Zanzibar imekuwa ikiongezeka kila mwaka. Katika mwaka huu wa 2015, taasisi zinazosafirisha mahujaji hapa Zanzibar kutokana na uongozi bora na uzoefu wa kuzifanya shughuli za Hijja za Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana zimeweza kusafirisha mahujaji 1,502, kati ya mahujaji 3,000 waliosafirishwa kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Idadi hii ni ziada ya mahujaji 222 ikilinganishwa na idadi ya mwaka jana ambapo taasisi za Zanzibar zilisafirisha mahujaji 1,280 kati ya 2,500 kwa Tanzania nzima.  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewekewa fursa ya kupeleka katika Hijja,  mahujaji 25,000 kwa mujibu wa makubaliano ya OIC.  Ni dhahiri kuwa idadi ya mahujaji wetu kwa sasa ni ndogo ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika ya Mashariki.  Aidha, imebainika kuwa mahujaji wetu wengi wanaokwenda Hijja ni watu wa hali za kati na hali za chini kiuchumi. Wengi wao huifanya ibada hii baada ya kupata fedha zao za kiinua mgongo.
Kwa lengo la kuwasaidia wananchi wengi zaidi waweze kupata fursa ya kuitekeleza ibada ya Hijja kwa wepesi na mapema zaidi, tayari Serikali imeanza kazi ya kufanya upembuzi yakinifu ili kuanzisha Mfuko wa Hijja Zanzibar. Mfuko huo utakapoanzishwa, watu wengi zaidi watapata nafasi na uwezo wa kuweka fedha kidogo kidogo kwa mujibu wa uwezo wao. Hatimae, watamudu kutekeleza ibada za Hijja na Umra kwa mujibu wa makubaliano na taratibu zitakazowekwa na mfuko.  Nchi nyingi ambazo zimeanzisha mifuko ya aina hii ikiwemo Malaysia, wanamudu kumaliza idadi yote ya nafasi za mahujaji walizowekewa.
Bila ya shaka, kwa kupitia utaratibu wa mfuko huu, mahujaji wetu watapata uwezo wa kufanya maandalizi mazuri ya misafara ya Hijja. Kadhalika, kwa miezi yote Waumini wengi watapata nafasi ya kwenda kutekeleza ibada za Umra na ziara.  Mifuko hii pamoja na kuwawezesha Waislamu kuhiji husaidia sana shughuli za kidini na kijamii.  Tayari Kamisheni ya Wakfu ya Mali ya Amana kwa kushirikiana na Benki ya Kiislamu ya PBZ, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF), Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC), Umoja wa Taasisi za Hijja Zanzibar na wataalamu wa Uchumi na Utawala kutoka taasisi za kiislamu wanalifanyia kazi suala hili na  matarajio ni kuanza kufanya kazi kabla ya Hijja ijayo. Tumuombe Mwenyezi Mungu atufanyie wepesi katika kulitekeleza jambo hili la kheri.
Ndugu Wananchi,
Ibada ya Hijja waliyoitekeleza ndugu zetu mahujaji huko Makka ina mchango muhimu wa kukuza imani ya mja na uchamungu wake kutokana na mafunzo muhimu yanayotokana na ibada hiyo yenye historia ndefu tangu kwa baba wa Mitume Nabii Ibrahim (AS).
Miongoni mwa mafunzo muhimu ya ibada ya Hijja ni kudhihirika kwa umoja wa Waislamu duniani ambao wanakutanika katika Mji wa Makka kwa kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu. Umoja wa waislamu umebainishwa katika aya mbali mbali za Kurani ambapo katika aya 92 ya Surat Al-Anbiyaa, Mwenyezi Mungu ametuthibitishia hilo na kututaka tumuabudu Yeye kwa kusema,
“Hakika umma wenu huu ni umma mmoja tu, na mimi ni Mola wenu, basi niabuduni”.
Hali hii ya umoja, tunapaswa tuione umuhimu wake na tuiendeleze katika maisha yetu ya kila siku hasa sisi tunaoishi katika nchi moja na watu wa nasabu moja.  Sote tuna wajibu wa kuimarisha umoja wetu na kuepukana na masuala yote yanayohatarisha umoja na mshikamano wetu kwa lengo la kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu na kupiga hatua kubwa zaidi za maendeleo.
Ndugu Wananchi,
Jambo jengine muhimu linalotokea katika kipindi cha ibada ya Hijja ni Waislamu kutoka sehemu mbali mbali duniani kupata fursa ya kukutana na kujadili masuala yanayohusu maendeleo ya jamii ya kiislamu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na ustawi wa jamii.  Katika hali kama hii, masuala mengi ya msingi huzungumzwa na Waislamu wenye taaluma, maarifa, uzoefu na kubadilishana mawazo kwa njia ya majadiliano na kupata njia za kukabiliana na changamoto za maendeleo zilizopo.  Fatwa zinazotolewa miongoni mwa maulamaa wa kiislamu, huwa ni dira muhimu katika kuleta ustawi wa jamii zetu.
 Hili nalo ni jambo la kuliendeleza katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbali mbali zilizomo katika jamii yetu.  Majadiliano ni njia nzuri na ya pekee katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto zetu za maendeleo ndani ya jamii yetu.  Ni wazi kwamba, jamii haiwezi kupata maendeleo kama watu watakosa kushirikiana na kuaminiana.  Kwa hivyo, kwa kutumia maarifa yanayotokana na mafunzo ya Ibada ya Hijja ni miongoni mwa faida tunazozipata katika utekelezaji wa Ibada hii na ni wajibu wetu tuyatumie mafunzo hayo katika maisha yetu ya kila siku.
Ndugu Wananchi,
Vile vile, katika ibada ya Hijja  tunajifunza umuhimu wa mahujaji kuwa  na subira na kwa wale tunaobaki nasi huwa tunawasubiri ndugu, jamaa na marafiki zetu waliokwenda kuitekeleza ibada hii kwa lengo la kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu.  Ibada ya Hijja inajumuisha taratibu nyingi pamoja na ugumu wa safari, gharama na haja ya kuwa na uzima wa afya na ustahamilivu.  Yote haya yanahitaji kuwa na subira ambayo ni sifa muhimu ya Mitume yote na Masahaba.  Kwa wale wanaoondokewa na ndugu na jamaa zao kwa ajili ya kwenda kuitikia wito huo wa Mwenyezi Mungu nao hulazimika kuwa na subira.
Kuwa na subira ni jambo lililosisitizwa sana katika Kurani na Sunnah kupitia visa vya Mitume wa Mwenyezi Mungu na Masahaba ili iwe ni mafunzo kwetu.  Katika kusisitiza faida ya kuwa na subira kwa muumini, Bwana Mtume (S.A.W) katika hadithi iliyopokelewa na Al-Bukhaariy na Ahmad amesema:
“Kubakia katika subira kwa siku moja katika njia ya Mwenyezi Mungu ni bora zaidi kuliko dunia na vyote vilivyomo ndani yake”
Ni dhahiri kuwa kuna fadhila kubwa katika kusubiri kwa siku hizi ambazo wenzetu wanatekeleza ibada ya Hijja huko Makka na sisi tunaowasubiri tukiwaombea dua ili ibada zao zikubaliwe.  Aidha, masheikh wetu wanatuelekeza kuwa subira yenye malipo zaidi ni ile ya kusubiri kwa kujizuwia kutekeleza mambo mabaya kwa kutegemea malipo mema kutoka kwa Mola wetu Subhana Wataala.  Tumuombe Mwenyezi Mungu atupe subira kwa kutegemea fadhila na kufuata maamrisho ya Mola wetu.
Ndugu Wananchi,
Miongoni mwa masuala muhimu tuliyosuniwa katika sikukuu hii ya Idd el Hajj ni kuchinja mnyama.  Uchinjaji huu unatupa funzo la utiifu wa Nabii Ibrahim (AS) na kutawakali kwake pamoja na mwanawe Ismail (AS) katika kutekeleza amri ya Allah kupitia ndoto aliyooteshwa.  Utiifu wao wa kweli kwa Mwenyezi Mungu uliwawezesha kufuzu, jambo ambalo la mazingatio kwetu sote na kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika masuala yetu mbali mbali ya kimaisha.
Mafundisho ya uislamu yanasisitiza umuhimu wa kuitekeleza suna hii ambayo ni ibada na hatua ya kumkurubisha mja na Mola wake.  Siku hii ya leo imesuniwa kuchinja mnyama baada ya sala ya Idd na kutumia sehemu ya nyama na nyengine kuwapa marafiki na wahitaji wengine waliokuwa hawana uwezo katika jamii.
Ni wajibu wetu kuyaendeleza mambo kama haya ya kheri na uchamungu ili iwe ni sababu ya kukuza mapenzi mema baina yetu na kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu kwa kufanya anayoyaridhia na kujiepusha na makatazo yake.  Kadhalika, tuendelee kuyatumia mafunzo yanayotokana na ibada zetu kwa vitendo ili iwe ndiyo dira ya kuleta ufanisi katika maisha yetu ya kila siku. 
Ndugu Wananchi,
Tuna wajibu mkubwa wa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kutuwezesha kuungana na waislamu wenzetu duniani katika kuisherehekea sikukuu hii ya Idd el Hajj katika hali ya amani na salama.  Nimepata faraja kubwa kuweza kushirikiana na waislamu wenzetu wa Mkoa huu wa Kaskazini Unguja kwa kusali pamoja sala ya Iddi leo asubuhi katika kiwanja cha mpira cha Polisi Mkokotoni na hivi sasa kwa pamoja tumejumuika katika kituo hiki cha Mafunzo ya Amali kwa ajili ya Baraza la Iddi.
Natoa shukurani zangu na naipongeza Kamati ya Maandalizi kwa kushirikiana vyema na uongozi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja pamoja na Wilaya zake katika kuifanikisha shughuli hii.  Kadhalika, nawapongeza kwa dhati wananchi wote wa Mkoa huu kwa kujitokeza kwa wingi katika sala ya Idd na kwa mashirikiano yenu mnayoendelea kutupa. Tumuombe Mwenyezi Mungu azidishe ushirikiano huu katika kuifanikisha mipango yetu ya maendeleo na kuimarisha ustawi wa wananchi wote.
Ndugu Wananchi,
Nimefarajika na hatua kubwa ya maendeleo tuliyoyafikia katika Mkoa huu wa Kaskazini Unguja katika sekta za kiuchumi, huduma za jamii na muamko wa wananchi katika kuzitumia fursa mbali mbali za kujiendeleza kiuchumi kwa kushirikiana na Serikali.  Napenda nikupongezeni sana kwa mafanikio hayo.
Katika kuhakikisha kuwa, Mikoa yetu inazidi kuimarika kiuchumi, kuongeza fursa za ajira hasa kwa vijana na kuimarisha upatikanaji mzuri wa huduma za jamii, Serikali imeazimia kujenga mji wa kisasa katika Mkoa huu wa Kaskazini kwenye vijiji vya Kijini na Matemwe.  Ujenzi wa barabara wenye urefu wa kilomita 20.2 kutoka Matemwe kupitia Kijini hadi Kidoti umekwishaanza. Wananchi wa Mkoa huu wananufaika na kuwepo kwa idadi kubwa ya hoteli za kitalii kwa kuzingatia kauli mbiu ya utalii kwa wote.
Ndugu Wananchi,
Inatia moyo kuona vijana na kinamama wa Mkoa huu walivyojidhatiti kujiendeleza kiuchumi kwa kutengeneza bidhaa mbali mbali na kuzalisha mazao kwa ajili ya kuuza katika Hoteli za kitalii.  Aidha, wananchi wengi wa maeneo ya Bumbwini, Mkokotoni, Bwekunduni, Fungurefu na vijiji nyengine vya Mkoa huu wameimarisha uchumi wao kwa kujishughulisha na biashara ya madagaa ambayo nimearifiwa kuwa husafirishwa hadi Kongo na nchi nyengine za jirani.
Wito wangu kwenu ni kuwa muendelee kushirikiana na Serikali yenu katika kuziimarisha shughuli zetu hizi ili ziweze kutoa tija zaidi.  Kadhalika, vijana wanaokosa fursa ya kuendelea na masomo wakitumie kituo cha Mafunzo ya Amali cha Mkokotoni ili wajiendeleze kupata ujuzi wa kazi mbali mbali za amali unaotolewa na kituo hicho.  Kazi hizo ni pamoja na useremala, ushoni, uchoraji, uwashi, ufundi bomba, magari, mafriji, mapishi ya aina mbali mbali na huduma za mahoteli.  Vile vile, katika mwezi wa Agosti, 2015 tulifungua kituo cha ujasiriamali “Bare-foot College” kama kiliopo huko India, kituo kinachotengeneza vifaa vya umeme wa jua ndani ya Mkoa huu ambacho ni cha aina yake na maalum kwa kinamama.  Hizo ni fursa ambazo mnapaswa kuzitumia vyema katika kupiga hatua zaidi za maendeleo.
Ndugu Wananchi,
Serikali kwa kushirikiana na washirika wetu wa maendeleo pamoja na ushirikiano wa wananchi tumeweza kupiga hatua kubwa katika kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Mkoa huu kwa kutekeleza miradi mbali mbali.  Hali ya upatikanaji wa maji safi katika Mkoa huu imefikia asilimia 71.68.  Mafanikio hayo yamefikiwa baada ya kutekeleza miradi mikuu mitatu ya maji safi na salama katika Mkoa huu.  Miradi hiyo ni mradi wa Serikali kupitia Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Mradi wa Maji wa Ras-al-Khaimah na Mradi wa Maji wa ADB ambayo kwa pamoja imewanufaisha wananchi mbali mbali wa Mkoa huu kupata huduma za maji safi na salama.   
Kadhalika, Serikali imeimarisha huduma za hospitali ya Koteji ya Kivunge pamoja na vituo vya afya vyengine katika Mkoa huo ili kuziimarisha afya za wananchi.  Wajibu wa wananchi ni kuzitumia huduma hizi pamoja na wazazi na walezi kuhakikisha watoto wetu wanapelekwa kupata chanjo ili kuwakinga na maradhi mbali mbali na kinamama wajawazito wawe wanajifungulia hospitali katika azma ya kuziimarisha afya zao.
Ndugu Wananchi,
Pamoja na mafanikio hayo katika kuziimarisha huduma za jamii, napenda nitumie fursa hii, kuutaka uongozi wa Mkoa wa Kaskazini; Unguja kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi pamoja na taasisi zinazowasimamia madereva wachukue hatua madhubuti katika kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani katika Mkoa huu. Taarifa kutoka Jeshi la Polisi zinabainisha kazi kubwa tuliyo nayo katika kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani.  Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika kipindi cha kuanzia mwezi wa Januari hadi Agosti mwaka 2014, jumla ya ajali za barabarani 391 zimetokea Unguja na Pemba.  Ajali hizo zilizosababisha vifo vya watu 104 na watu 728 wamejeruhiwa.  Katika Mkoa huu wa Kaskazini Unguja zilitokea ajali 64 zilizosababisha vifo vya watu 16 na jumla ya watu 259 walijeruhiwa. 
Katika mwaka huu wa 2015 kwenye kipindi kama hicho, tayari zimetokea ajali za barabarani 393 Unguja na Pemba ikiwa ni ziada ya ajali mbili ikilinganishwa na mwaka 2014.  Ajali hizo zimesababisha vifo vya watu 91 na watu 450 wamejeruhiwa.  Katika kipindi hiki kwenye Mkoa huu, kumetokea ajali za barabarani 73, zilizosababisha vifo vya watu 15 na kuwajeruhi watu 123.  Ni wazi kuwa takwimu hizo si za kufurahisha, kwa hivyo jitihada za pamoja zinahitajika ili kupunguza na hatimae kuliondoa kabisa tatizo la ajali za barabarani kwa vile asilimia kubwa ya ajali hizi zinasababishwa kwa kutokuzingatiwa kwa sheria za usalama barabarani na matumizi mazuri ya barabara zetu. 
Ndugu Wananchi,  
Kwa mara nyengine napenda nikumbushe umuhimu wa sisi viongozi wa kisiasa, kijamii na wa madhehebu ya dini kuwasisitiza wafuasi wetu umuhimu wa kuilinda amani na kujiepusha na vitendo vyote vinavyoweza kutuondolea amani na utulivu tuliokuwa nao.  Nimekuwa nikisema mara kadhaa kuwa amani haina mbadala.  Bila ya amani hatuwezi kupata maendeleo yoyote.  Kutokuwepo kwa amani kunahatarisha uhai wa watu na ni sababu ya kuharibu miundombinu ya aina mbali mbali na kuzua fadhaa katika jamii.  Ni dhahiri kuwa kutoweka kwa amani huwaondolea wasaa hata waumini katika kutekeleza ibada za kumuwabudu Mola wao.  Katika aya ya 112 ya Suratun Nahl, Mwenyezi Mungu anatutanabahisha kwa kutupa mfano wa waliopewa neema ya amani na utulivu wakashindwa kuitunza kwa kusema:
“Na Mwenyezi Mungu anakupeni mfano wa mji uliokuwa na amani na utulivu, riziki yake ikiujia kwa wingi kutoka kila mahali.  Lakini ukazikufuru neema za Mwenyezi Mungu, kwa hivyo Mwenyezi Mungu akauvika vazi la njaa na khofu kwa sababu ya yale waliyokuwa wakiyafanya”.
Tumuombe Mwenyezi Mungu atuepushe na mtihani huo. 
Napenda nikuhakikishieni kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitaendelea  kukabiliana na wale wote watakaofanya vitendo vinavyoashiria kutaka kuvunja amani ya nchi yetu wakati wote na katika kipindi hiki cha Kampeni za Uchaguzi Mkuu, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.  Hakuna atakayeonewa au kudhulumiwa kwa njia yoyote ile lakini Serikali ina wajibu wa kikatiba wa kuwalinda watu wote na mali zao pamoja na wageni wanaoitembelea nchi yetu. 
Ndugu Wananchi,
Hivi sasa tumo katika kusherehekea sikukuu, lakini kama tunavyofahamu baada ya siku chache zijazo tunatarajia kuanza kupata baraka za mvua za Vuli.  Mvua ni neema kubwa kwetu hasa kwa kuendeleza shughuli za kilimo na upatikanaji wa maji nchini. Kwa hivyo, ni vyema tukaanza maandalizi ya kilimo cha mazao na matunda mbali mbali yanayostawi na kunawiri katika msimu wa Vuli. 
Kwa upande mwengine, ni muhimu tukazingatia kwamba baadhi ya nyakati, Mwenyezi Mungu hutupa neema ya mvua ambayo vile vile huwa na mitihani ili kuzipima nafsi zetu. Mwenyezi Mungu ametuambia katika Surat Muhammad aya ya 31 kwamba:
“Nitakufanyieni mitihani mpaka muwadhihirishe (wajulikane) wale wanaopigania dini miongoni mwenu, na wanaosubiri nasi tutadhihirisha habari zenu”. 
Sote tunakumbuka jinsi baadhi ya wananchi wenzetu walivyopata mitihani ya mafuriko katika sehemu mbali mbali za Unguja na Pemba katika msimu wa mvua za Masika uliopita. Tulishuhudia matukio mengi ya kusikitisha katika maeneo ya Kwahani, Mwanakwerekwe, Tomondo na kadhalika, katika mwezi Mei, 2015.  Mimi na viongozi wengine tulipata fursa ya kuwatembelea wananchi waliopata maafa kwa ajili ya kuwafariji. 
Napenda niwakumbushe wananchi kwamba katika nyakati mbali mbali, Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini “Tanzania Meteorological Agency (TMA)”, imetahadharisha kwamba katika msimu wa mvua za Vuli, upo uwezekano mkubwa wa kutokea mvua kubwa za “El-Nino” kutokana na hali ya sasa ya kuongezeka kwa joto katika Bahari ya Pasifiki. Ongezeko hilo la joto katika bahari hiyo kama litaendelea kuwepo, linaweza kuenea hadi katika Bahari ya Hindi na kusababisha mvua kubwa za “El-Nino” katika ukanda wote unaopakana na bahari ya Hindi. 
Kwa kawaida mvua kubwa za “El-Nino” zinapolikumba eneo la nchi husababisha mafuriko na kuacha madhara makubwa ya uharibifu wa miundombinu na mali za wananchi; hasa nyumba zilizojengwa katika maeneo ya mabondeni.  Wataalamu wetu wanatufahamisha kwamba kuna viasharia vingi sana vya kuonesha uwezekano wa mvua za “El Nino” kutokea mwaka huu katika Ukanda wa Afrika Mashariki. 
Huu ni utabiri wa binaadamu lakini Mwenyezi Mungu ana kudra na shani yake. Utabiri huu unatokana na elimu na maarifa aliyotupa Subhana Wata’ala, ili kurahisisha maisha yetu. Ni vyema tukaitumia elimu hii vizuri kwa kuanza kuchukua tahadhari zinazofaa. Nasaha zangu kwenu wananchi ni kwamba tuzingatie hekima ya ule usemi maarufu kwamba, “Tahadhari kabla ya athari”.  Kwa hivyo, taasisi zinazoshugulikia usafi wa miji ziongeze kasi katika kusafisha misingi ya maji machafu na njia za maji, usafi wa mazingira yetu ili kuepukana na maradhi.  Ninawanasihi wananchi tuache ujenzi katika sehemu za mabonde na sote tuwe na moyo wa kusaidiana wakati wote, hasa pale Mwenyezi Mungu anapotupa mitihani mbali mbali. 
Ndugu Wananchi,
Kwa baraka ya siku hii, tuwaombee mafanikio vijana wetu wa darasa la sita, la saba na Kidato cha Pili waliofanya mitihani yao hivi karibuni na Mwenyezi Mungu awape matayarisho mema vijana wetu wanaojiandaa na mitihani ya Taifa Kidatu cha Nne. Awajaalie wote wafaulu katika mitihani yao.  Awape wagonjwa wetu wote shifaa ya maradhi yao na aijaalie nchi yetu amani, upendo na masikilizano na mapenzi zaidi baina yetu. 
Namalizia hotuba yangu kwa kukuombeeni nyote kila la kheri katika kuisherehekea sikukuu hii ya Idd-el-Hajj.  Tuisherehekee sikukuu hii kwa mambo ya kheri na kujiepusha na yale yote yanayomchukiza Mwenyezi Mungu.  Tumuombe Mwenyezi Mungu azikubali ibada za mahujaji wetu wote.  Tunapowasiliana nao tuwaombe waiombee nchi yetu iendelee kuwa ya amani na utulivu. Mwenyezi Mungu awape uwezo wale wote wenye azma ya kuitekeleza ibada ya Hijja waweze kufanya hivyo kama walivyokusudia na kupata fursa ya kuishi japo kwa siku chache katika miji mitukufu ya Makka na Madina Yarabbil Allamina  
Mwenyezi Mungu awarehemu wazee wetu, ndugu, jamaa na marafiki zetu wote waliotangulia mbele ya haki. Aijaze neema na baraka nchi yetu. Atupe uwezo na wepesi wa kuitekeleza mipango yetu ya maendeleo kama tulivyoipanga.  Atujaalie afya njema na riziki za halali. Mwenyezi Mungu atujaalie sote turudi nyumbani kwa salama na amani.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.
IDD MUBARAK
KULLU AAM WAANTUM BIKHEIR

Rais wa  Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein akipena mkono wa  Eid na wananchi mbali mbali
katika  khafla ya Eid mkokotoni  Zanzibar.

Rais wa  Zanzibar Dr  Ali Mohamed  akipena mkono na watoto kutoka sehemu mbalimbali za Zanzibar waliofika Mkokotoni kujumuika pamoja katika Eid .

Wananchi mbalimbali maelf kwa mael waliomiminika Mkokotoni kuungana na Rais wa  Zanzibar kwenye swala  ya Eid.
Rais wa  Zanzibar Dr  Shein akiwa kwenye mahojiano na watoto kwenye khafla ya  Eid Mkokotoni
Rais  wa  Zanzibar Dr  Ali Mohamed  Shein akisalimaian na kupeana mkono wa Eid  na kinamama  waliohudhuria khafla  ya  Eid  Mkokotoni  Zanzibar.
Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed  Shein akisherehekea sikukuu ya Eid na wananchi kwa aina yake kwa kucheza  bao . Bao ni mchezo wa asili wa utamaduni wa mwahili wa mwambao wa Afrika Mashariki.
Ahsanteni sana  wananchi wa  Jimbo  la  Tunguu Wilaya ya  Kati Mkoa wa Kusini wa  Unguja kwa kuja  kwa  wingi  kwenye  uwanja wa  mpira wa Bungi kumsikiliza mgombea urais wa  Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein leo hii 21.Sept 2015.
Mgombea  urais wa  Zanzibar kupitia  CCM Dr Ali  Mohamed  Shein akiwahutubia wananchi maelf  kwa maelf walifurika aktika uwanja wa mpira wa  Bungi kwenye  mkutano wa kampeni leo. 
Waziri Kiongozi mstaafu amabe  pia mjumbe  wa  Kamati Kuu  ya  Chama  Cha  Mapinduzi Mhe.  Shamsi  Vuai  Nahodha akiwahutubia wananchi na kuwataka  wapime  ukweli  na uongo , kisha  wachague  ukweli.

Balozi  Amina  Salum  Ali akiwahutubia  wanachi waliofika  kwenye mkutano  huo.
 




 
 



 




















Mgombea  Urais Dr Ali Mohamed akiwanadi  wagombea   udiwani wa CCM katika  Jombo hilo  





Ahsanteni sana  wananchi wa Jimbo la Micheweni  Wilaya  ya Micheweni Mkoa wa  Kaskazini Pemba kwa kuja  kwa  wingi  kwenye  uwanja wa  mpira wa Konde kumsikiliza mgombea urais wa  Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein leo hii 19.Sept 2015.

 DK. SHEIN AHUTUBIA MKUTANO WA KAMPENI MICHEWENI NA KUSEMA:
·         Wavuvikaenimkaowakulaneemainakuja
·         Wakulimawamwani mambo yenubombakabisa
Mgombeanafasiyauraiswa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameahidi ndani ya miaka miwili kukamilisha mpango mkubwa wa kuimarisha  sekta ya uvuvi utakaojumuisha kuwapatia wavuvi boti maalum za kufanyia shughuli za uvuvi. Amesema mpango huo ambao matayarisho yake tayari yameanza utashirikisha sekta binafsi ambapo tayari makubaliano ya awaliyamefanyika ambapo katika hatua ya awali boti 20 kumi zikiwa za mita 6 na nyingine 10 za mita 9 zitapewa wavuvi kwa majaribio. Akizugumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kiwanja cha Shamemata huko Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dk. Shein alieleza kuwa endapo wavuvi watazikubali boti hizo baada ya majaribio boti nyingine zaidi zitatengenezwa na kupewa wavuvi.Dk. Shein alifafanua kuwa baada hatua hiyo kukamilika itafuata hatua nyingine ya ujenzi wa boti za ukubwa wa zaidi ya mita 18 kwa ajili ya uvuvi wa bahari kuu hivyo kutoa fursa kwa wavuvi wa Zanzibar kuvuna rasilimali hiyo muhimu kwa uchumi wanchi. “Tunaamini kuwa tunaweza kuwawezesha kuvua samaki eneo la bahari kuu ndani ya miaka mitano kwa kushirikiana na kampuni moja kubwa ya kutengeneza boti na meli za uvuvi ya Sri Lanka” Dk. Shein aliwaambia wananchi hao waliokuwa wakimshangilia kwa nguvu sana.
Mgombea huyo aliwahakikishia wakulima wa mwani kuwa serikali imejidhatiti kuhakikisha kuwa kilimo cha mwani aina ya ‘cotton’ wenye thamani zaidi ambao majaribio yake yalifanyika katika baadhi ya vijiji vya wilaya ya Micheweni kinaimarishwa. Aidha Serikali atakayoiunda akichaguliwa tena itawapatia ndani ya miaka mitano kinamama wakulima wa mwani vihori 500 vya kubebea mwani baada ya serikali kuwapatia vihori 100 mwanzo ni mwa mwaka  huu. “Nimekamilisha ahadi zangu kwenu kuhusu barabara, maji na afya na kuhusu hili la uendelezaji wa eneo huru la kiuchumi la Micheweni limeshafanyiwa usanifu tayari kwa utekelezaji” Dk. Shein alibainisha.

  

Mgombea  Urais  wa  Zanzibar  kupitia  CCM  Dr  ALi Mohamed akisalimiana  na  maelf  ya  wananchi  waliokuwa  na  hamu kupoeana  mikono na yeye baada  ya kumaliza mkutano.


 
 















Ahsanteni sana  wananchi wa Jimbo la  Konde Wilaya  ya Micheweni Mkoa wa
 Kaskazini Pemba kwa kuja  kwa  wingi  kwenye  uwanja wa  mpira wa Konde kumsikiliza mgombea urais wa  Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein leo hii 18.Sept 2015.


DK. SHEIN AWAAMBIA NWANANCHI:NICHAGUENI NIA YANGU NI KUIBADILI ZANZIBAR HATUA KWA HATUA
·         MkinichaguanitaheshimuKatiba na SheriakwakuundaSerikaliyenyeMfumowaUmojawaKitaifa.

MgombeaUraiswa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi  Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi kumchangua tena kwa mara ya pili kuongoza Zanzibar ili aweze kutekeleza dhamira yake ya kuendelea kuibadili Zanzibar hatua kwa hatua.
Akizungumza katika mkutano mkubwa wa kampeni katika mji mdogo wa Konde katika Wilaya Micheweni,MkoaKaskazini Pemba leo mgombea huyo amesema “amekusudiakuibadili Zanzibar hatuakwahatua”.
Aliwaambia wananchi hao kuwa Serikali aliyoiongoza ambayo ilikuwa chini ya mfumo wa Umoja wa Kitaifa ilifanya kazi nzuri na kuiwezesha Zanzibar kujenga mazingira mazuri ya kuimarisha uchumi wake.
Katika mkutano huo Dk. Shein ambaye pia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anaemaliza muda wake alisema akichaguliwa tena ataheshimu Katiba na Sheria kwa kuunda Serikali iliyo katika Mfumo wa Umoja wa Kitaifa kama Katiba inavyoelekeza.
Aliahidi wananchi wa Konde kuwa katika kipindi kijacho pamoja na kuwa kumekuwepo na mafanikio makubwa katika kusambaza huduma za jamii serikali itaendelea kuimarisha huduma hizo.
Dk. Shein aliwatahadharisha  vijana kuhusu kauli rahisi za wanasiasa zinazoeleza kama kwamba suala la ajira ni jambo jepesi na kuwaeleza kuwa serikali haina uwezo wa kutoa ajira kwa kila kijana lakini kinachofanyika ni kuweka mazingira mazuri ili vijana wengi waweze kujiajiri.

 
 
 
Ahsanteni sana ndugu  wananchi wa Pemba kwa kuja  kwa  wingi  kwenye  uwanja wa  Chokocho Black Magic kumsikiliza mgombea urais wa  Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein leo hii 17.Sept 2015.  


Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein  amesema kuwa katika uongozi wake ametekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa vitendo huku pia, akitekeleza vizuri uongozi wake katika Serikali yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa kwa amani na utulivu.

Dk. Shein ambaye ni Mgombea nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM aliyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa kwenye mkutano wa Kampeni wa chama hicho uliofanyika huko katika viwanja vya Gombani ya Kale, Chake Chake Pemba.
Dk. Shein aliwaeleza maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa endapo atachaguliwa tena ataendelea kuimarisha utulivu, amani na kuendelea kuwahudumia wananchi wa Zanzibar bila ya ubaguzi wa aina yeyote iwe wa kidini, rangi, kabila na hata mahala kwani hayo ndio maelekezo ya chama chake. 
Alitaja baadhi ya mafanikio ya uongozi wake kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha ukuaji wa uchumi kutoka asilimia 4.5 hadi 7.2  ambapo kwa upande wa pato la taifa limeongezeka hadi trilioni 1.508 kutoka trioni 2.138.
Kuhusu mfumuko wa bei kiwango alisema kitaendelea kushuka ikiwa ni uthibitisho wa kutengemaa kwa uchumi wa taifa huku akieleza mipango uendelezaji wa maeneo huru ya Kiuchumi ya Fumba kwa kujengwa mji mpya pamoja na viwanda.
Kupambana na umasikini, kituo cha kulelea wajasiriamali ambacho ni kikiubwa katika Afrika Mashariki, ni lazima kuweko na programu maalum na hakuna njia ya mkato kama inavyoelezwa na Wapoinzani.
Aidha, Dk. Shein alieleza mafanikio yaliopatikana katika sekta ya kilimo na kueleza azma yake ya kuendeleza sekta hiyo huku akisisitiza kuendelea kutoa ruzuku na kuendelea kuwasaidia wakulima.
Kwa upande wa karafuu, alisema kuwa uwamuzi wa kuinua zao la Karafuu ni utekelezaji wa Ilani ya CCM na kwamba hatua zilizochukuliwa la kutolibinafsisha biashara ya zao hilo sambamba na kupandisha bei ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kuimarisha zao hilo nchini.
Dk. Shein alibainisha kuwa uamuzi huo ulifanywa nan yeye mwenyewe na kupewa baraka na Baraza la Mapinduzi na kumtuma Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko kutanganza uamuzi huo.
Alisema kuwa asilimia 80 ya bei ya karafuu duniani wamepewa wakulima huku akieleza kuwa uongozi ni kazi na zaidi ni kuonesha njia.
Hadi sasa alieleza jumla ya tani za karafuu 5340 zimeuzwa na kukomesha magendo ya zao hilo kwa kuhakikisha kuwa taratibu zinafuatwa katika kuuza karafuu na hatua inayochukuliwa hivi sasa ni kuzifanya karafuu za Zanzibar kuwa alama maalum'branding'.
Katika sekta ya barabara Dk. Shein alieleza mafanikio yaliofikiwa kisiwani Pemba na hakuna barabara hata moja inayoungana na barabara kuu za Pemba ambayo haina lami na zilizobaki zinatarajiwa kumaliza karibuni.
Katika kuimarisha miundombinu ya usafiri wa baharini alieleza kuwa bandari mpya ya Mpigaduri itakayokuwa na uwezo wa kushughulikia kotena 200,000 kwa kwa mwaka itaanza kujengwa mara baada ya kukamilika kwa jengo la uwanja wa ndege.
Aidha  aliongeza kuwa Bandari ya Wete itajengwa upya na kuwaomba wananchi wawe wastahamilivu. 
Kwa upande wa wafanyakazi wa Serikali aliwaahidi kuendelea kuiamarisha maslahi yao kama alivyofanya katika kipindi chake cha uongozi kinachomalizika huku aliahidi endapo atachaguliwa tena atapandisha kima cha chini cha mshahara hadi 300,000 kwa mwezi.
kuhusu utekelezaji wa Ilani ya CCM alisema utekelezaji umefanyika kwa asilimi 90 ambapo asilimia iliyobaki itaenaendelea kutekelezwa huku akieleza jinsi juhudi zilivyochukuliwa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd nae alipata nafasi na kusikitishwa na maneno ya uongo yanazotolewa na kiongozi wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad.
Balozi Seif alisema kuwa Dk. Shein amefuata Ilani ya CCM kwa kuongeza bei ya karafuu pamoja na kuongeza idadi ya miche ya mikarafuu sambamba na kuliimarisha zao hilo. 
Alisema kuwa chama cha CUF hakina uzoefu wa kuendesha Serikali na kueleza kuwa Maalim atakuwa mtu maarufu kwa kugombania mara sita urais wa Zanzibar huku akieleza kuwa mwisho wa chama chake ni 2015 kwani chama hicho na yeye mwenyewe hawatoweza kufikia mwaka 2020. "2015 CUF itakufa kifo cha mende miguu juu",alisema Balozi Sif.
Aliwata Wana CCM kuendelea kushikamana na kuwa wamoja kwa lengo la kupata ushindi wa uhakika  huku akisisitiza kuwa CCM ikishinda na Maalim Seif akikataa matokeo Dk. Shein ataunda Serikali ya CCM pekee.
Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai, alisema kuwa wananchi wa Pemba mwaka huu wamedhamiria na wataleta mabadiliko makubwa. 
Alieleza kusikitishwa na tabia za viongozi wa CUF za kuwatuma watoto pamoja na vijana kuchana picha za wagombea wa CCM zilizobandikwa huku akivitaka vyama vyote kufanya siasa za kistaarabu. 
Nao viongozi wa CCM walipata fursa ya kusalimiana na wananchi pamoja na WanaCCM waliohudhuria katika mkutano huo na kuwapongeza wananchi wa Pemba kwa kuonesha azma ya kukiunga mkono chama hicho.
Mohamed Aboud nae alieleza kuwa chama cha CUF kimemuweka rehani  Makamu Mwenyekiti wao Juma Duni kwa kujiunga na CHADEMA na kusisitiza kuwa hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo nongono kuwa Maalim Seif amechoka na nafasi ya Makamu wa Kwanza na anataka kupewa Juma Duni na ndipo akaamua kumpeperusha na kumpelekeka CHADEMA.
Kiongozi huyo alilaani hatua iliyochukuliwa na CUF ya kuwatoa viongozi wao katika Baraza la Wawakilishi huku akieleza athari za kutoka kwao katika kikao hicho ambacho kilikuwa kinapitisha Bajeti ya Serikali.
Alieleza kuwa katika kipindi cha miaka mitano Dk. Shein amefanya kazi kubwa sana katika kuleta mabadiliko makubwa na kujenga misingi imara ya maendeleo na anafaa kuwa Rais, na kuwahakikishia Wazanzibari kuona Zanzibar mpya katika uongozi wake wa miaka mitano ujao kwani ana mipango kabambe ya  kuondosha  umasikini na kuongeza ajira kwa vijana.
Nae Balozi Ali Karume aliwaomba wananchi wa Pemba kumpa kura zao Dk. Ali Mohamed Shein kutokana na kuwa na uwezo, uzoefu na kueleza kuwa mgombea wa CUF hamfikii Dk. Shein.
Bi Mauwa Daftari nae alieleza mafanikio yaliopatikana katika kuimarisha miradi ya maendeleo ikiwemo maji, barabara, umeme na mengineyo na kueleza jinsi anavyomfahamu Dk. Shein kuwa ni muadilifu, mchapakazi na hana tabia ya kusema uongo.  Alisema kuwa Sera za CCM ni kuwasikiliza wananchi shida zao na kuzifanyia kazi huku akisema anamfahamu sana Dk. Magufuli kwani amefanya kazi nae pamoja na sifa zake zinafanana  na za Dk. Shein na kueleza kuwa akipigiwa Dk. Shein akina mama nao tayari wameshapata nafasi kupitia Mama Samia Suluhu Hassan. 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Hamad Mberwa, akiwakaribisha viongozi na WanaCCM pamoja na wananchi katika Mkoa huo alisema kuwa Pemba ya mwaka 1995,2000 na 2010 sio ya leo na wananchi wake wamebadikila, kimawazo na kivitendo. Kampeni rasmi za CCM zilifunguliwa siku ya Jumaapili tarehe 13.





 
Ahsanteni sana ndugu  wananchi wa Pemba kwa kuja  kwa  wingi  kwenye  uwanja wa  Gombani ya Kale kwenye uzindizi wa kampeni ya mgombea urais wa  Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein leo hii 15.Sept 2015.  Shein
Mgombea  urais wa  Zanzibar kwa  CHAMA CHA MAPINDUZI dr. Ali Mohamed  Shein akizungumza na Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Ng. Vuai Ali mara  baada ya kuwasili Uwanja wa Gombani  ya Kale  leo hii  Pemba.
Mgombea  Urais Dr  Ali Mohamed Shein akiowaonesha Katiba ya CCM wananchi waliohudhuria kwenye mkutano 
Mgombea  Urais  Dr  Ali Mohamed  Shein akiwahutumia maelf ya wananchi wa  Pemba  waliokuja kusikiliza sera zenye kutekelezeka za  Chama  Cha  Mapinduzi katika uzinduzi wa kampeni Pemba.

DK. SHEIN:TUTAWANYOA KIPARA WAPINZANI
·         Asema:Mkinichaguandani yamwaka mmoja kima cha chini cha mshahara kitakuwa laki tatu.
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi kuendelea kukiamini chama hicho kwa kuwa ni chama makini kilicho na mipango madhubuti inayotekelezeka na ndio sababu Ilani yake ya uchaguzi imeweza kutekelezwa kwa zaidi ya asilimia tisini.
Amewaeleza maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika katika kiwanja cha Gombani ya Kale kisiwani Pemba kuwa akichaguliwa tena ataendelea kuweka mazingatio katika suala la kuendeleza amani na utulivu kama alivyofanya katika kipindi kilichopita.
Kwa hivyo aliwakumbusha na kuwaasa wananchi kuacha chokochoko zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani na kusisitiza kauli yake ya mara kwa mara kuwa watu wa Zanzibar ni wamoja hivyo hawapaswi kufarakana badala yake waimarishe udugu wao kwa salama na amani kwa maslahi ya nchi yao.
Dk. Shein alitumia mkutano huo kuielezea Ilani ya CCM katika kipindi kijacho cha uongozi na kuwaeleza wananchi kuwa wanayo kila sababu ya kumuunga mkono yeye na chama chake kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010-2015.
Alibainisha kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake kiwango cha ukuaji wa uchumi kimeongezeka kutoka asilimia 4.3 kwa mwaka hadi asilimia 7.2 hivi sasa wakati mapato ya serikali yaliongezeka kutoka shilingi bilioni 181.9 mwaka 2010/2011 hadi shilingi bilioni 360.4 mwaka 2014/2015.
Katika kipindi hicho alisema pato la mwananchi mmoja mmoja limeongezeka hadi shilingi milioni 1.56 kwa mwaka.
Kwa mwenendo huo wa uchumi ulioambatana kushuka mfululizo kwa mfumko wa bei alieleza kuwa ni ishara ya mwelekeo mzuri wa uchumi na kuleta matumaini ya kufikia lengo la Dira ya Zanzibar ya kuifanya Zanzibar kuwa nchi yenye uchumi wa kiwango cha kati ifikapo mwaka 2020.
Alisema awamu ijayo kama alivyofanya awamu iliyopita ataongeza kasi ya kuongeza ajira kwa kupanua wigo wa shughuli za kiuchumi ikiwemo kujenga miradi mipya ya kiuchumi itakayotoa ajira nyingi.
Alisisitiza nafasi za ajira hazizuki tu kwa ahadi hewa bali ni mipango mizuri inayotekelezeka na kufanikishwa kwa ufanisi jambo ambalo linaweza kutekelezwa na serikali inayoongozwa na CCM.
Dk.shein alikanusha maelezo ya viongozi wa Chama cha Wananchi –CUF kuwa uamuzi wa kupandisha bei ya karafuu ulifanywa na chama hicho na kuwataka wananchi kutowasikiliza viongozi wa aina hiyo wanaofanya ulaghai katika kuomba kura.

Endapo akichaguliwa, Dk. Shein aliahidi kuongeza kima cha chini cha mshahara kutoka shilingi 150,000 za sasa hadi shilingi 300,000.
BALOZI SEIF ALI IDDI AMSHUKIA MAALIM SEIF.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi amesema jitihada za Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi-CUF za kutaka urais wa Zanzibar zitaishia redioni tuna kamwe hazitafanikiwa.
Aliwaeleza wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni huko Gombani ya Kale nje kidogo ya mji wa Chake-Chake kuwa kiongozi huyo pamoja na chama chake hawana sifa wala uzoefu wa uongozi nchi.
Alisema Chama cha Mapinduzi pekee ndicho chenye viongozi wanaoweza kushikadola na ndio maana chama hicho kimekuwa na utaratibu wa kubadilisha wagombea tofauti na CUF ambayo imekuwa na mgombea mmoja tu wa nafasi ya urais katika chaguzi zote tangu mwaka 1995 hadi mwaka huu ikiwa mara ya tano.
Alisema baada ya uchaguzi kumalizika kiongozi huyo ataingia katika vitabu vya kumbukumbu vya‘Guinness’ akiwa kiongozi aliyesimama kugombea nafasi ya urais mara nyingi duniani na mara zote amekuwa akishindwa.
Balozi Seif alikanusha maelezo ya baadhi ya viongozi wachama cha CUF kuwa Chama cha Mapinduzi hakina watu Zanzibar na kueleza kuwa jibu lake watalipata Oktoba 25.
“Si vyema kwa kiongozi wa chama kuwapotosha wananchi ili wampe kura ilihali akijua anayoyasema si kweli” alieleza Balozi Seif.
Aliwaonya viongozi wa CUF kwa kutumia kauli hizo za hadaa katika kutafuta kura na kutolea mfano kauli za Katibu Mkuu wa chama hicho ambaye ni mgombea urais kupitia chama hicho kuwa meli mpya iliyonunuliwa na serikali pamoja jengo jipya la kiwanja cha ndege Zanzibar atayazindua yeye wakati atakapokuwa Rais wa Zanzibar kitu ambacho sio kweli.
Balozi Seif aliwaeleza wananchi kuwa katika miaka 5 inayomalizika Dk. Shein aliongoza serikali iliyo katika mfumo wa Umoja wa Kitaifa kwa mafanikio makubwa lakini viongozi wa upinzani wanawadanganya wafuasi wao kuwa serikali haijafanya kitu. 
 MOHAMED ABOUD:WANANCHI PEMBA WAMEIKUBALI CCM
·         CUFhawaijui mipango ya CCM.
·         Imewakwama ndoano hawatoki lazima waisome namba.
 Mjumbe wa Kamati ya CCM ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed amesema wananchi wa Pemba wameonesha hamasa mpya ya kukiunga mkono Chama cha Mapinduzi na hiyo imedhihirisha maneno yaliyokuwa yakisemwa kwa miaka mingi kuwa Chama cha Wananchi-CUF si chama.
Alisema mwamko mkubwa waliouonesha wananchi wa Pemba kukiunga mkono Chama cha Mapinduzi umewatia homa wapinzani na wameanza kutapatapa.
Mheshimiwa Aboud alihoji umakini waviongozi chama cha CUF wa kumpeleka kiongozi wake wa ngazi ya juu kwenye chama kingine badala ya kubaki kuongoza na kutumikia chama chake.
Kwa hivyo alibainisha kuwa uamuzi wa CUF kumpeleka Makamu Mwenyekiti wake Juma Duni UKAWA unadhihirisha uvumi kuwa kuna mgogoro katika chama hicho unaohusisha nafasi ya kugombea urais kupitia chama hicho.
Alifafanua kuwa minong’ono kuwa Maalim amechokana Juma Duni angalau angeweza kusimama nafasi ya urais matokeo yake ni kupelekwa rehani Juma Duni huko UKAWA na hiyo inatosha kuthibitisha kuwa chama hicho ni cha mtu mmoja.
Aidha alieleza kuwa kilichomfanya Juma Duni kukubali kuwekwa rehani UKAWAni fedha na uroho wa madaraka na si kitu kingine.
Aliwakosoa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Chama hicho kwa kitendo chao cha kukacha vikao muhimu vya Baraza kitu kilichodhihirisha kuwa chama hicho hakiko kwa maslahi ya nchi wala hakijali wananchi wanaodai kuwawakilisha.
“Kukacha kikako cha bajeti kunadhihirisha dhamira mbaya waliyonayo wenzetu wa CUF kwa wananchi na Zanzibar na kinachodhihiri zaidi choyo chao dhidi ya mafanikio yaliyoletwa na serikali chini ya uongozi wa Dk. Shein” alieleza Mhe Mohamed Aboud.
Kutokana na wananchi wa Pemba kuwabaini CUF kuwa hawana nia njema na wananchi wala dhamira nzuri kwa nchi yao basi lazima waisome namba.
“CUF imeshawakwama ndoana hawakujua mipango ya CCM lazima wataisoma namba Oktoba 25” alisemza Mjumbe huyo na kusisitiza mgombea wa CCM Dk. Ali Mohamed Shein ndio “jembe la maendeleo Zanzibar.”
Aliwataka wamchague Dk. Shein na kuwahakikishia wananchi kuwa katika miaka mitano ijayo watashuhudia Zanzibar mpya kutokana na mipango mizuri iliyopangwa na mazingira bora yaliyowekwa na serikali ya Dk. Shein.
BALOZI KARUME: WANANCHI MSIHANGAIKE, RAIS TUNAYE.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi Balozi mstaafu Ali Karume amewataka wananchi wasihangaike kutafuta Rais wa Zanzibar kwa kuwa tayari wanaye.
“Nimesimama kumuombea kura Dk. Ali Mohamed Shein, uwezo anao na uzoefu anao,tusikae majukwaani kutafuta Rais wakati Rais yuko tayari” Balozi Karume alisema.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kiwanja cha Gombani ya Kale nje ya mji wa Chake Chake Balozi Karume alisema katika kuwaangalia wagombea amepima na kugundua kuwa mpinzani wa Dk. Shein katika nafasi hiyo Maalim Seif hana sifa na hawezi kulinganishwa nae.
Alibainisha kuwa mwaka 2011 Maalim Seif alimrai Balozi Karume ajiunge na Chama cha Wananchi-CUF lakini alimkatalia.
“aliponitaka nijiunge na CUF nikamwambia kinagaubaga kuwa sijaona kipya kilichofanywa na chama hicho wala sijaona baya lililofanywa na CCM” Balozi Karume aliueleza mkutano huo.
Aliongeza kuwa alimpasulia Maalim kwa kumueleza kuwa wakati wa mkoloni asingepata fursa ya kugombea urais na kama angethubutu kutamka neno hilo angefungwa jela.
Ni kutokana naMapinduzi ya mwaka 1964 ndio leo anathubutu kugombea urais hivyo anapaswa kuheshimu Mapinduzi badala ya kuyabeza na pia kuheshimu na kuenzi muungano wa Zanzibar na Tanganyika.
“Msikosee kuwapa madaraka hawa jamaa watatuletea mambo yasiyotarajiwa.Nchi zinazoongoza kwa maendeleo hivi leo zilipitia kwenye Mapinduzi na baadae kwenda katika Muungano” Balozi Karume aliwaambia wananchi na kusisitiza kuwa Mapinduzi na Muunganowetu ni lazima kuuenzi na kuyaendeleza.


Umati wa wanaccm  Pemba  waliokuja kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni ya mgombea  urais wa Zanzibar.
Ahsanteni sana ndugu  wananchi kwa kuvunja  rekodi kwa kujaza mafuriko kwenye  uwanja wa  Demokrasia na hii ni historia ambayo  haijawahi kutokea. maana yake  ni Ushindi kwa  Dr  Shein.
Mgombea  Urais wa  Zanzibar  wa  CHAMA CHA MAPINDUZI  Dr  Ali Mohamed  Shein akiwahutubia wananchi waliohudhuria kwa wingi mno katika  Uwanja wa Demokrasia katika ufunguzi wa kampeni ya Urais.
Mwenyekiti wa CHAMA CHA MAPINDUZI  . DR JAKAYA KIKWETE akimkabidhi Ilani ya  CCM mgombea  wa Urais wa  Zanzibar  Dr  Ali  Mohamed  Shein katika  ufunguzi wa kampeni Uwanja wa  Demokrasia .
Mwenyekiti wa  CCM Dr Jakaya Kikwete akiwahutubia  wananchi waliohudhuria mkutanoni.
Makamu wa  Rais Dr Mohamed  Gharib  Bilal akiwahutumia  wananchi katika  mkutano  huo.
Makamu wa Pili wa Rais wa  Zanzibar  Balozi  Seif  Ali Idi akiwahutubia wananchi waliofika .
Naibu  Katibu Mkuu CCM  Zanzibar Nd Vuai Ali akiwahutubia wananchi .
Katibu Mkuu wa  CCM Nd. Abdulrahman Kinana akiwahutubia  wananchi .
Rais  mstaafu Bw. Ali Hassan Mwinyi akiwahutumia  wananchi 
Rais  mstaafu  Bw.  Benjamin Mkapa akiwahutubia  wananchi.

WALIOCHUNGULIAA  KWENYE  VIOO VYA NDEGE  ZILIPITA  JANA  KWA JUU MKUTANONI WALIO HIVI. ANGALIA  CHINI TAFADHALI.








WALIOCHUNGULIAA  KWENYE  VIOO VYA NDEGE  ZILIPITA  JANA  KWA JUU MKUTANONI WALIO HIVI.
 
MGOMBEA URAIS ZANZIBAR DR ALI MOHAMED  SHEIN AKIUNGUMZA  NA UMOJA WA WANAFUNZI WA  VYUO VIKUU VYA ZANZIBAR 
Sababu 40 za Dk. Ali Mohamed Shein kugombea tena nafasi ya Urais wa  Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed Shein ameamua kugombea tena nafasi ya Urais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kupitia Chama Cha Mapinduzi. Uamuzi wake huo unatokana na kwanza dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Zanzibar na pili, kuitikia wito wa wazee wa CCM na wananchi wa Zanzibar. Pamoja na sababu hizo, ziko sababu nyengine 40 kubwa zinazomshawishi kila mtu kukubali kwamba uamuzi wa Dk. Shein ni sahihi. Kwa ujumla sababu hizo na nyenginezo ndizo zilizokipelekea Chama Cha Mapinduzi kumteua kupeperusha bendera yake katika uchaguzi mkuu ujao. Sababu hizo ni:-
1.     Ameonesha uwezo mkubwa wa kusimamia na kutekeleza  Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 – 2015 kwa zaidi ya asilimia 90.
2.     Katika kipindi chake cha uongozi ameimarisha uchumi kutoka asilimia 6.0 mwaka 2010 hadi asilimia 7.4  mwaka 2014 na kuongeza kasi ya maendeleo.
3.     Ameinua kiwango cha ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo yameongezeka kutoka TZS bilioni 181.4 hadi kufikia TZS bilioni 360.4, sawa na ukuaji wa asilimia 98.7 kwa kipindi cha mwaka 2010/2011 hadi 2014/2015 au wastani wa asilimia 19.7 kwa kila mwaka.
4.     Amepelekea kupungua kwa mfumko wa bei kutoka asilimia 14.7 mwaka 2010  hadi asilimia 5.6 mwaka 2014 na kwenda sambamba na maelekezo ya Ilani ya kutaka kufikia chini ya asilimia 7.
5.     Kwa kuimarika uchumi, Pato la Taifa kwa mwananchi mmoja, kwa bei za miaka 2010 – 2014, limekua kutoka TZS 856,000 ($613) mwaka 2010 hadi kufikia TZS 1,552,000 ($939) kwa mwaka 2014 ikiwa imepita lengo la Ilani la shilingi 884,000 kwa mwaka 2015.
6.     Wakulima kunufaika na ruzuku za pembejeo za kilimo kulikopelekea kuongezeka kwa mazao hasa ya mpunga, mboga mboga na mifugo, ambapo zaidi ya wakulima 360,000 wamefaidika.
7.     Kuwaondoshea kodi wananchi kwa bidhaa muhimu kama vile sukari, mchele na unga wa ngano.
8.     Kuliimarisha zao la karafuu kwa kulireshea hadhi, heshima na kulipa nafasi yake katika uchumi wa Zanzibar.
9.     Amewaongezea uwezo wakulima wa zao la karafuu pamoja na kuongeza bei ya zao hilo kwa wakulima kutoka shilingi 4,500 mwaka 2010 hadi kufikia shilingi 14,000 mwaka 2014 kwa kilo moja.
10.         Amepindukia lengo la Ilani ya Uchaguzi katika ujenzi wa barabara kwa kujenga kilomita 431.6 kwa kiwango cha lami badala ya kilomita 356.3 zilizomo kwenye Ilani.
11.         Kwa kushirikiana na sekta binafsi ameimarisha huduma za usafiri wa baharini pamoja na kupanua maeneo ya kuhifadhia makontena na zana za kisasa za ukaguzi wa mizigo.
12.         Amesimamia ununuzi wa meli mpya ya kisasa ya abiria na mizigo katika kukabiliana na tatizo la usafiri kati ya Unguja, Pemba na Dar es Salaam.
13.          Amesimamia na kutekeleza kwa ufanisi mkubwa mpango wa upanuzi na uendelezaji wa kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume pamoja na kiwanja cha ndege cha Pemba.
14.         Amekamilisha mradi wa umeme unaopita chini ya bahari kutoka Ras Kiromoni wa Megawati 100, pamoja na kutekeleza kwa ufanisi mradi wa usambazaji umeme vijijini vikiwemo baadhi ya visiwa vidogo vidogo.
15.         Amefanikiwa kuongeza kwa kasi huduma za usambazaji wa maji safi na salama kutoka asilimia 75 mwaka 2010 hadi asilimia 87 kwa maeneo ya mjini na kutoka asilimia 60 mwaka 2010 hadi asilimia 70 kwa upande wa vijijini.
16.         Amewaondoshea wazee mzigo wa kuchangia ada ya skuli katika ngazi ya elimu ya msingi ili kuhakikisha kwamba fursa sawa ya elimu inapatikana kwa watoto wote bila ya kujali kipato chao.
17.         Amesimamia juhudi za kuongeza ujenzi wa skuli na madarasa kulikopelekea kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaorodheshwa katika ngazi zote za maandalizi, msingi, sekondari na vyuo vikuu.
18.         Ameweka mazingira mazuri ya kuweka uwiano wa kijinsia katika utoaji wa elimu kwa ngazi zote na kutoa fursa zaidi kwa wanawake. Kwa mfano, katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) idadi ya wanafunzi wa kike imeongezeka kutoka 853 mwaka 2010 kati ya wanafunzi 1972 hadi wanafunzi   1244 mwaka 2015 kati ya wanafunzi 2078 ikiwa ni zaidi ya wanafunzi wa kiume.
19.         Ameimarisha miundombinu ya afya ikiwemo majengo, wataalamu na vifaa vya kisasa.
20.         Ameimarisha huduma za kinga na tiba na huduma ya mama na mwana katika hospitali na vituo vya afya mijini na vijijini ikiwa ni pamoja na kuondoa malipo kwa akinamama waja wazito wanaokwenda hospitali kujifungua.
21.         Amesimamia hadi kukaribia kufikia kiwango cha kimataifa cha daktari mmoja kutibu watu 8000 ambapo kwa Zanzibar daktari mmoja amefikia kutibu watu 9000. 
22.         Amewanufaisha wananchi kwa kuanzisha mpango wa utalii kwa wote na kuimarisha sekta hiyo kulikopelekea kuongeza idadi ya watalii kutoka 132,836 mwaka 2010 hadi kufikia 311,891 mwaka 2014.
23.         Amefanya safari za nje zenye tija na maslahi makubwa kwa Wazanzibari ambapo matunda ya ziara hizo yameongeza kasi ya uwekezaji na kukuza ajira.
24.         Ameiwezesha Zanzibar kuingia katika ramani ya kimataifa kihabari kwa kuitoa katika mfumo wa analogia na kuingia katika mfumo wa kisasa wa digitali.
25.         Ameimarisha miundombinu mbali mbali ya michezo ikiwemo kuifanyia ukarabati mkubwa viwanja vya michezo vya Amani na Gombani ili iweze kutumika kwa mashindano mbali mbali ya kimataifa,  pamoja na kukijenga upya Kiwanja cha Mao - Tse Tung.
26.         Amesimamia kurejeshwa hadhi ya viwanja vya kufurahishia watoto Unguja na Pemba kuvijenga upya na kuweka vifaa vya kisasa.
27.         Kuinua viwango vya mishahara ya watumishi wa umma na sekta binafsi  pamoja na kuimarisha maslahi yao kwa ujumla.
28.         Msimamo wake usiyoyumba katika kuimarisha amani, utulivu na maelewano miongoni mwa Wazanzibari.
29.         Msimamo wake usiyoyumba wa kuuendeleza na kuudumisha Muungano wa Serikali mbili.
30.         Makini na hayumbi katika kutetea jambo analoliamini kulingana na katiba na sheria za nchi.
31.         Ana uwezo mkubwa wa kufanyakazi bila ya kuchoka na kujali wakati.
32.         Mkweli na mchapakazi hodari, asiyekubali fitna wala majungu, hana ubinafsi, ana uchungu wa Zanzibar na watu wake hasa wanyonge.
33.         Ameonesha umakini na uhodari mkubwa katika kuasisi na kuongoza serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa kitaifa.
34.         Kuchukia viongozi na watumishi wanaokiuka maadili ya uongozi, sheria na kanuni za utumishi wa umma.
35.         Kukerwa na vitendo vya rushwa vinavyofanywa na wanaotoa na wanaopokea rushwa na ndio sababu ya kupitisha sheria ya kupambana na rushwa na uhujumu wa uchumi.
36.         Ameithibitishia jamii kwamba anachukia vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa watoto na watu wazima.
37.         Ameweka mkazo mkubwa katika kukamilisha dhamira ya kuendeleza maeneo huru ya uchumi, mpango ambao ulibuniwa tokea mwaka 1993.
38.          Juhudi maalum alizozichukua katika kuzifanyia kazi zile zinazotambuliwa kuwa kero za muungano, ambapo  masuala kadhaa yameshatatuliwa kupitia Kamati inayoongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayowajumuisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
39.         Amewajali sana wazee kwa kuwahudumia, kuwatunza, kuyaimarisha makaazi yao, kuwapatia huduma muhimu za kila siku kwa maisha yao na kuwawekea posho  maalum kwa kila mwezi.
40.         Amekusudia  kuibadilisha taswira ya eneo la Fumba baada ya kukamilika Mradi wa Ujenzi wa Mji wa Kisasa wa Fumba ambayo utekelezaji wake unaendelea pamoja na Mradi unaoendelea wa Maendeleo ya Mji wa Kisasa Kijini – Matemwe katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.




No comments:

Post a Comment